Hassani Kessi Yupo Tayari Kurudi Tanzania Kuitumikia Yanga

Jina la beki la pembeni Mtanzania anayekipiga Klabu ya Nkana ya nchini Zambia, Hassan Kessy, limejadiliwa na Kamati ya Usajili ya Yanga na kukabidhiwa kwa Kocha Mkuu Mbelgiji, Luc Eymael huku Kessy mwenyewe akisisitiza kuwa yupo tayari kujiunga Yanga.

Kessy ni kati ya wachezaji wanaotajwa hivi sasa kuwaniwa na Yanga katika kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu Bara ambao timu hiyo imepanga kukisuka kikosi chao ili kichukue makombe.

Beki huyo ni mchezaji huru hivi sasa kwa mujibu wa kanuni za Fifa kutokana na mkataba wake kumalizika Agosti, mwaka huu, hivyo anaruhusiwa kufanya mazungumzo na klabu nyingine itakayomhitaji.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumatatu, Yanga inataka kumsajili beki huyo kwa ajili ya kuiboresha safu hiyo ya beki ya pembeni inayochezwa hivi sasa na Juma Abdul na Paul Godfrey ‘Boxer’ ambaye hana nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza.

Mtoa taarifa huyo alisema kuwa kocha ndiye aliyependekeza usajili wa beki wa pembeni katika kuiboresha na Kessy ndiye aliyependekezwa na baadhi ya viongozi wa Yanga.

Aliongeza kuwa jina la Kessy tayari limekabidhiwa kwa kocha ambaye yeye ataamua asajiliwe au vipi, hivyo kama akikubali basi haraka atapewa mkataba wa miaka miwili.

“Kessy ndiyo jina la kwanza la beki wa kulia lililopendekezwa na mabosi wa Yanga ambao tayari wamempatia kocha ambaye yeye ndiye atakayeamua hatima yake.

“Kocha anamtaka beki mwenye uwezo na uzoefu wa kucheza michuano ya kitaifa na kimataifa, hivyo upo uwezekano mkubwa wa Kessy kusajiliwa na Yanga,” alisema mtoa taarifa huyo.

Alipotafutwa Kessy kuzungumzia hilo alisema: “Mimi mkataba wangu unatarajiwa kumalizika mwezi Agosti, hivyo nipo tayari kujiunga nayo kwani nimepata taarifa za kunihitaji, lakini bado hawajanifuata kiofisi.”

45 Komentara

    Hapa yanga wanatakiwa wasipoteze muda kama Kessy alikuwa kwenye kiwango kizuri basi ni wakati wa kumjumuisha kwenye kikosi chao ili kuleta upinzani

    Jibu

    Safii Sana habari nzuri

    Jibu

    Kessy yanga ni safi kurudi huko ulipokua kama kumedumaza kiwango chako

    Jibu

    Safi sana wachangamkie fursa hyo fasta

    Jibu

    Kama angekua yupo kwenye form nzuri nkana ya Zambia ingemuongezea mkataba hamna kitu hapo.

    Jibu

    Karbu sana nyumbn Ni nyumbn

    Jibu

    Bora aluji ajekuikomboa yangaa maana mmmh

    Jibu

    Ni habar njema sana kwa mashabiki wa yanga kuona bek wetu amerud tena kufanya Kaz kwan Tanzania kwa ujumla tunatambua uwezo wake
    Baada ya kuonyesha uwezo mkubwa, uongozi wa Moro Kids kama kawaida yao ulifanya mazungumzo na wenzao wa Mtibwa Sugar kwa lengo la kumsajili Kessy kwenye timu yao ya vijana ili kuanza kupata uzoefu.
    Mtibwa Sugar walimsajili Kessy msimu wa 2011 aliitimikia timu hiyo hadi mwaka 2014, ndipo Simba walipomuona baada ya kucheza mechi ya Ligi Kuu ambayo kocha Mecky Mexime alimtumia na kuonyesha kiwango kikubwa.
    Alitua Simba msimu wa 2014 kwa mkataba wa miaka miwili ambapo, hakupata changamoto ya namba kwani aliyekuwepo kwa wakati huo, Emiry Nimubona, raia wa Burundi hakuwa kwenye kiwango bora.
    Msimu wa mwisho mwa 2016, Kessy alijiunga Yanga kwa mkataba wa miaka miwili ambao, ulimalizika mwaka jana, 2018 na kujiunga Nkana Rangers ya Zambia inayoshiriki Ligi Kuu nchini humo kwa mkataba wa miaka miwili. Akiwa Nkana ameshiriki michuano ya kimataifa ya Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho Afrika.
    Hivyo tunatarajia tena kumuona kujiunga na club ya wananchi

    Jibu

    Itakuwa vizuri km akirudi yanga.

    Jibu

    Imekaapoa hii

    Jibu

    Jabari njema sana izii

    Jibu

    Arud tu nyumban

    Jibu

    Habari njma kwa mashabiki Wake pamoja & yanga afrika#

    Jibu

    Arud tu nyumban nafas yake ipo pale Jangwan

    Jibu

    Acha arudi aokoe jahazi maana yanga hawapo sawa

    Jibu

    Arudi tu

    Jibu

    Kweli TZ tunavipaji sawa akuje tu yanga

    Jibu

    Kalb mwamba

    Jibu

    Rudi bwana maana yanga inakaribia kufa kabisa

    Jibu

    Hana jipya Tena uyo angekuwa ni mahili nkana wangeendelea kubaki nae yanga nao wanasajili tu ovyo wanabidi ndo timu itakuwa imara kumbe wanapoteza
    Izo pesa wanazozitumia kusajili watu ni Bora wangewapatia wachezaji waliopo Ili wapate moyo wa kucheza kwa juhudi zote

    Jibu

    Hana jipya Tena uyo angekuwa ni mahili nkana wangeendelea kubaki nae yanga nao wanasajili tu ovyo wanadhani ndo timu itakuwa imara kumbe wanapoteza
    Izo pesa wanazozitumia kusajili watu ni Bora wangewapatia wachezaji waliopo Ili wapate moyo wa kucheza kwa juhudi zote

    Jibu

    Inabidi yanga wasipoteze muda kumsajili kiungo huyo katika kikosi chao

    Jibu

    Nihabari njema

    Jibu

    Karibu sana kwani nyumbani ni nyumbani#meridianbettz

    Jibu

    Ni habari njema

    Jibu

    Habari njema kwa mashabiki wake

    Jibu

    Yanga inahitaji nafkiri kukisuka kikosi chake chote namaanisha kwenye idara zote kwani timu haipo vizuri kabisa,Kessy kurudi nae atakuja kuwasaidia sana

    Jibu

    Natumai wana yanga watakuwa wameipokea vizur hii habari…hongera kwao wana yanga

    Jibu

    fursa iyo

    Jibu

    habar njema sana kwa mashabiki wa yanga kuona bek wetu amerud tena kufanya Kaz kwan tuna matumaini kuwa kikosi chetu kitakuwa imara zaidi ukiangalia kwa hasaivi tunategemea kupata wachezaji wa nnje wa 5 wa ndani 4 ambao wanajua mpinda wa kimataifa ambao wanaweza kuisuka yanga ikawa iko katika kiwango kizuri zaidi .

    Jibu

    Habari njema kwa mashabiki wa nyanga kupata beki mzuri na mwenye viwango vya juu

    Jibu

    saf

    Jibu

    Arudi tuu maana wanayanga wako vibaya kwakweli

    Jibu

    Karibu tena yanga hassan kesi mashabiki wa simba wataongea sana lakini kwa vile wew mwenyew hunaonesha bado damu yako hipo yanga mtoto kurudi kwao sio mbaya naona wengi hawajui umetokea wapi wanaongea ongea tu

    Jibu

    Habari njema kwa mashabiki wa yanga

    Jibu

    Nalo ni Jambo zuri Kama atarudi ili kuiokoa timu take ya zamanii

    Jibu

    Habari nzuri kwa yanga

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    habari njema bora arudi kuisaidia yanga

    Jibu

    Saafi sana

    Jibu

    Kama Nkana hawajaonyesha nia ya kuendelea nae inawezekana hana kiwango cha kutisha. Timu zetu zinapaswa kusajiri watu watakaoleta mafanikio katika timu#meridianbettz

    Jibu

    Aludi kuisaidia yanga

    Jibu

    asije akazingua kama Morrison

    Jibu

    huyu ana nin mbona anapenda shida jaman

    Jibu

    Hii ni habari njema

    Jibu

Acha ujumbe