Henry Ajiondoa Kwenye Mitandao ya Jamii Kisa Ubaguzi.


 

Mchezaji wa zamani wa Arsenal, Thierry Henry anasema anajiondoa kweye mitandao ya kijamii hadi unyanyasaji na ubaguzi utakapodhibitiwa “kwa nguvu na ukali ule ule” ambayo ukiukaji wa hakimiliki unafanyika.

Henry, ambaye hivi karibuni aliachana na kazi ya kukinoa kikosi cha Montreal Impact, na anataka uwajibikaji kutoka kwa makampuni ya mitandao ya kijamii.

 

Thiery Henry ambaye amewahi kuchezea Arsenal, Barcelona na New York Red Bulls aliandika kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii:

“Kuanzia kesho (Jumamosi) asubuhi nitajiondoa kwenye media ya kijamii hadi pale watu walio madarakani watakapoweza kudhibiti majukwaa yao kwa nguvu na ukali sawa. ambazo zinafanya sasa unapokiuka hakimiliki.”

Katika taarifa kwa Sky Sports News, msemaji wa kampuni ya Facebook alisema:

“Hatutaki unyanyasaji wa kibaguzi kwenye Instagram na tunauondoa tunapoipata. Kati ya Oktoba na Desemba mwaka jana tulichukua hatua kwa vipande milioni 6.6 vya matamshi ya chuki kwenye Instagram, asilimia 95 ambayo tulipata kabla ya mtu yeyote kutuarifu.

“Hivi majuzi tulitangaza kuwa tutachukua hatua kali tutakapogundua watu wanaovunja sheria zetu katika DM na tumeunda zana za kusaidia watu kujilinda.”


Maana Kamili ya Ushindi Katika Kasino za Meridianbeti ni Pamoja na Mchezo wa Tropical Wild.

Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Tropical Wild na uwe moja ya washindi na Mabingwa.

CHEZA HAPA

6 Komentara

    Kila mtu na maamuzi yake

    Jibu

    Amefanya vizuri henry kutilia mkazo swala la ubaguzi

    Jibu

    Duuh

    Jibu

    Ubaguzi sio poa

    Jibu

    Ubaguzi utaisha lini

    Jibu

    Jambo zur

    Jibu

Acha ujumbe