Gonzalo Higuain, 32, alipoteza mkwaju wa penalti katika mchuano wake wa kwanza ndani ya jezi za kikosi cha Inter Miami inayomilikiwa na mwanasoka wa zamani wa Manchester United, David Beckham.
Inter Miami walipokezwa kichapo cha 3-0 na Philadelphia Union katika mechi hiyo ya Major League Soccer (MLS) mnamo Septemba 27, 2020.
Higuain ambaye ni raia wa Argentina, alisajiliwa na Inter Miami mnamo Septemba 18, 2020 baada ya mkataba wake na Juventus ya Italia kutamatishwa.
Nyota huyo ambaye pia amewahi kuvalia jezi za Chelsea, alipaisha penalti aliyoaminiwa kupiga katika dakika ya 77.
Mechi hiyo ilikamilika kwa hisia kali baada ya Higuain kuzua vurugu kwa kumsukuma beki Jakob Glesnes aliyesherehekea bao la Philadelphia mbele yake.
Ingawa hivyo, kocha wa Inter Miami, Diego Alonso alieleza kuridhishwa na mchango wa Higuain katika mechi hiyo na kusisitiza kwamba mchezaji huyo atayaweka kando maruerue ya kupoteza penalti na kujipanga katika mechi zijazo.
Mabao ya Philadelphia yalifungwa na Anthony Fontana, Ilsinho na Brenden Aaronson.
Inter Miami kwa sasa wanashikilia nafasi ya 13 kwenye msimamo wa MLS Tawi la Mashariki kwa alama sawa na DC United. Philadelphia wanakamata nafasi ya pili kwa alama mbili pekee nyuma ya viongozi wa msimamo, Columbus Crew.
Beti kwa Kitochi Kushinda 300,000,000!
Unajua kuwa unaweza kushinda milioni mia tatu kwa buku tu? Ndiyo! Unaweza kushinda kwa kupiga *149*10# na kubashiri. Ingia mchezoni!
Elika
Kiukweli walianza vinasa sana inatakiwa wakae wayajutie makosa aliyoyafanya higuan
Rehema
Asante kwa taarifa
Adelta
Higuain pole sana ila usikate tamaa bado muda upo ongeza juhudi
Mwanahamisi
Higuain pole sana
magdalena
kuanza vibaya si kumalizia vibaya, anaweza akaanza vibaya na mwisho wa siku akamalizia vizuri
Dorophina
Inter Jana walipoteza mechi kwa uzembe wao walikuwa wanakosa magoli ya wazi kabisa
Angelina
Inter jana walianza vibaya kweli ila bado wana nafasi yakufanya vuzuri
Mwajumah
Poleni sana Higuain
Fatina mfigi
Poleni ila msikate tamaa!
Caroline
Pole yao
Lydia Emmanuel Magoti
Duu pole yake nyota huyo msimu kuwanza vibaya
Tatu
Higuain ameaza mchezo vibaya kwanza kukosa penat pili kutaka kuanzisha fujo ugenini asipoangali anaweza kuwekwa bench na club yake
Ester jackson
Poleni sana inter ila kuteleza sio kuanguka
Venerose
Pole sana
Khadija
Pole san inter
Ernest
Higuani anatakiwa kutulia tuu
Neema
Pole yao
Salma ngende
Bahati akiuwa yao
aisha
Pole yake
Nasra
Pole sana 💗
Sabrina
Duuh pole sana
Mariam mtandama
Duuuh
Samira
Pole yake
Saupha mohamed
Pole sana
felister
Higuan anatakiwa kutulia
Hidaya
Pole yake
Rose kapinga
Mwanzo mgumu!!
Amiri Kayera
Mpila umeisha akubali alud Argentina
David Pere
kuanza vibaya si kumalizia vibaya, anaweza akaanza vibaya na mwisho wa siku akamalizia vizuri
Sauda
Pole sana Higuain.
Zeiyana
Hayo ndio maisha ya mpira wanatakiwa wakubaliane na matokea tu
Hopemwaikuka
Jamanii
Povel
Duh majanga
Gabriel
anaweza akaanza vibaya na mwisho wa siku akamalizia vizuri
Samiah
Duuh