Kocha mkuu wa Kaizer Chiefs, Gavin Hunt ameonyesha kuwa na hofu na nyota wawili wa Simba SC, Luis na kiungo Clatous Chama kuelekea katika mchezo wa pili wa marudiano.
“Tunatakiwa kuwa bora katika kuwazuia viungo wao hasa yule wa Msumbiji (Miquissone) na Chama (Clatous), ni viungo ambao hawatakiwi kupewa nafasi ya kucheza kwa ubora wao.
“Simba ni timu ambayo imekuwa bora zaidi inapocheza nyumbani wanajiamini zaidi kupata matokeo wakiwa kwao na mashabiki wao inawezekana hiyo ikawa silaha yao kubwa muhimu ni sisi kuwa katika ubora wa kupata matokeo pia huko.” amesema Hunt.
Simba SC wana kibarua kizito cha kupindua kipigo cha matokeo ya 4-0 waliyopata katika Jiji la Johannesburg, South Africa katika mchezo wa kwanza uliopigwa jumamosi iliyopita.
Zungusha na ushinde mkwanja wako papo hapo baada ya mzunguko kukamilika. Ni kugusa tu 🤑.
Shakila
Simba wako juu
Magdalena
Ndo tegemeo lao kubwa
Sauda
Chama jembe