Huyu Ndiye Paul Scholes

Yule mwandishi alimsogelea tena Socrates ili amsikie vizuri, ni kama masikio yake hayakuamini alichokuwa anasikia.

“Si umeniuliza kiungo bora wa katikati kwa sasa duniani? Basi jibu langu halitabadilika, ni mvulana Fulani hivi mwenye nywele nyekndu, anavaa jezi nyekundu pale Manchester, Yule muingereza Paul Scholes. Nadhani anastahili kuichezea timu ya taifa ya Brazil.”

Hakuna aliyetegemea jibu kama lile kutoka kwa mchezaji wa Brazil. Wengi walisubiri amtaje Rivaldo, Ricardo Kaka au Gilberto Silva. Lakini yeye hakumuona kiungo wa Brazil kwenye jedwali moja na Scholes.

Gilberto Silva

Hadithi ya Scholes inaanzia mbali sana katika mashindano ya shule za sekondari Uingereza mwaka 1991. Hapo ndipo mabalaa yake yalionekana na kusajiliwa na academy ya Manchester United mwaka 1991.

Alipiga kazi sana katika timu ya watoto lakini aliachwa ‘kichwa chini akiishangaa ardhi’ Alipowashuhudia washikaji zake wakimuacha na kupandishwa timu ya wakubwa 1992.

Wanae David Beckham, Nicky Butt, Garry Neville,Ryan Gigs na Phil Neville, wote walimuacha akipangiwa ratiba ya kulala katika timu ya watoto, wao wakapanda kwenda kukipiga ‘theatre of dreams’.

Ilibidi asubiri mwaka mmoja mbele ili apandishwe timu kubwa. Akapandishwa na kukabidhiwa jezi namba 24.

Alilazimika kusubiri nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza iliyokuja baada ya Mark Hughes kujiunga na Chelsea na binadamu mkorofi kuliko wote ‘mfalme mtukutu’ Eric Cantona kupigwa rungu la kukaa nje ya uwanja kwa miezi nane baada ya kumgeuza shabiki begi la mazoezi ya ndondi, akamtupia teke kama wanacheza Kung fu.

Paul Scholes akapata nafasi ya kudumu iliyomuweka Manchester United kwa miaka 20. Pale Manchester amecheza mechi 718, amebeba jumla ya mataji 25 kati ya hayo mawili ya klabu bingwa Ulaya. Ametwaa mataji 11 ya Ligi kuu ya Uingereza, hakuna mchezaji wa Kingereza aliyefikisha idadi hiyo.

Ni Scholes huyu ambaye Zinedine Zidane na ufundi wake wote anakiri kwamba, hakuwahi kukutana na kiungo mgumu kama Paul Scholes. Hata Xavi Hernandez na pasi zake zote anadai kwamba hakuwahi kumuona kiungo aliyekamilika kama Scholes.


MALIZA MWAKA KIBINGWA KWA KUJISHINDIA SHEA YAKO KWENYE SHILINGI 140,000,000TSH!!

Kipindi hiki cha sikukuu kinamalizika kwa namna ya kipekee. Shilingi 140,000,000 kushindaniwa katika michezo ya Evolution kwenye Kasino Mubashara ya Meridanbet. Ingia mchezoni na ujiwekee nafasi ya kushinda shea yako!!!

SOMA ZAIDI

19 Komentara

    Hili ni bonge la makala

    Jibu

    Nice update

    Jibu

    Alikua ni kiungo matata Sana pale old tranford Wana man u hawana Budi kumkumbuka legendary kama paul kwa mambo aliyoyafanya kwenye career yake ya mpira.

    Jibu

    Hiko poa Sana hii

    Jibu

    Imeka poa sana

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Haina ubishi kwamba kazi yake ktkt ya dimba ilikuwa ya kutukuka mno, nilisikitika kwanini alistaafu wakati bado alikuwa na uwezo mkubwa!

    Jibu

    Iko poa

    Jibu

    Scholes hazuiliki

    Jibu

    iko poa

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Haina upizani kabisa

    Jibu

    Paul Scholes akapata nafasi ya kudumu iliyomuweka Manchester United kwa miaka 20. Pale Manchester amecheza mechi 718, amebeba jumla ya mataji 25 kati ya hayo mawili ya klabu bingwa Ulaya. Ametwaa mataji 11 ya Ligi kuu ya Uingereza, hakuna mchezaji wa Kingereza aliyefikisha idadi hiyo.

    Jibu

    Good

    Jibu

    Nlkua cmjui vzur

    Jibu

    Kiungo fund

    Jibu

    Kiungo mzuri

    Jibu

    Alikuwaga tishio

    Jibu

    Ilikua powa sana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.