Icardi Abakizwa PSG

Mabingwa wa ligi kuu ya Ufaransa ‘Ligue 1’, Paris Saint-German wamefanikiwa kumbakiza kikosini nyota wa timu ya taifa ya Argentina, Mauro Icardi na kumsainisha mkataba wa miaka minne. Dili hilo litamfanya Icardi aendelee kubaki PSG mpaka June 2024!

Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina aliyeitumikia PSG tangu mwezi wa tisa mwaka jana akiwa kama mchezaji wa mkopo kutokea Inter Milan, ameonesha kiwango cha kuridhisha ndani kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1, na tayari amefanikiwa kuingia katika muunganiko mzuri uliozaa utatu mtakatifu wa Yeye (Icardi), Neymar na kylian Mbappe kiasi cha kutosha kuwashawishi mabosi wa PSG kutoa kitika cha zaidi ya pauni 54m ili kuinasa saini yake.

Hapo awali iliripotiwa kuwa PSG wangetakiwa kutoa zaidi ya pauni 60m ili kumsajili jumla nyota huyo katika kikosi chao, lakini hilo limekwamishwa kutokana na matokeo ya mlipuko wa janga la Corona na athari zake katika uchumi wa vilabu mbali mbali duniani.

Mauro Icardi mwenyewe anaonesha kuwa na furaha ndani ya PSG na mara kadhaa amenukuliwa akikiri hilo, sio tu na waandishi wa habari lakini pia na waliokuwa mabosi wake akiwa Inter. “Yeye (Icardi) anataka kuendelea kubaki PSG, sisi kama timu tupo katika mazungumzo ili kufanikisha hilo”, alinukuliwa Piero Ausilio, mkurugenzi wa michezo wa Inter Milan akisema kabla dili hilo halijakamilika.

Mpaka sasa nyota huyo wa Argentina ameshacheza jumla ya mechi 31 na kikosi cha PSG huku akiingia kambani mara 20! Icardi amekuwa mbadala sahihi kabisa wa nyota Edinson Cavanni aliyekuwa akiandamwa na majeraha.

35 Komentara

    ningeshangaa kama PSG wangemuondoa kikosin Icard, hili pia ni jembe ambalo linamsaada sana pale PSG

    Jibu

    Kama kweli atabaki PSG itatisha sanaa msimu ujao

    Jibu

    huu ni uamzi mzuri kwa Icardi maana kutokuelewana na maboss zake wa zamani pale international Milan hakukuwa na afya kwa kazi yake

    Jibu

    Icard mchezaji amestahili kupewa mkataba wa kudumu hapo PSG#meridianbettz

    Jibu

    Ni maamuz mazur sana kumbakiza kwn icardi kwn cavan hatambulik Kama hatasalia thnks kwa update za michezo na burudani

    Jibu

    Icardi amejtaid kwa kiasi chake

    Jibu

    Maamuzi mazuri kubaki PSG maana ataangeenda Inter angekaa benchi tu wakati Icardi nimchezaji mzuri sana

    Jibu

    Safi Sanaa

    Jibu

    Kutokana na icardi kuenyesha uwezo wake PSG wanastahil kumfanya abaki tu coz anamchango mkubwa sana

    Jibu

    Icardi really deserve it.

    Jibu

    Psg ilitakiwa kumpa mkataba wa maisha icardi coz Ni mchezaji mzuri sana

    Jibu

    Safii sana

    Jibu

    Icardi ndio jembe la PSG

    Jibu

    Dili hilo litamfanya Icardi aendelee kubaki PSG

    Jibu

    Ikopoa Kama kweri atabaki PSG itatisha Sana msimu unaho kuja huo

    Jibu

    PSG wataendelea kutisha Ligue 1

    Jibu

    PSG bila Icardi hakuna kitu

    Jibu

    Icard yupo poa Sana na kaipa jina PSG

    Jibu

    Icardi kwa Psg ni sehemu mzr kwake .magoli 20 kwa mechi 30 ni jinsi gani anavyoonesha kwamba anastaili kubaki

    Jibu

    Aendelee kubaki sababu ni mchezaji mahiri sana na PSG inamuamini sana

    Jibu

    Jembe hilo libakie tu psg

    Jibu

    uamzi mzuri kwa Icardi maana kutokuelewana na maboss zake wa zamani pale international Milan hakukuwa na afya kwa kazi yake

    Jibu

    Abak Psg tu

    Jibu

    Abaki PSG kwana anaipenda kutoka moyoni nafikili msimu unao kuja atafanya maajabu makubwa

    Jibu

    PSG imefanya maamuzi mazuri

    Jibu

    Bwana mtu asikwambie kizuri kizuri tu, Icardi mchezaji hodari

    Jibu

    Mauro Icardi mwenyewe anaonesha kuwa na furaha ndani ya PSG amefanya kitu kinzuri sana nimeipenda hii

    Jibu

    Dili hilo litamfanya lcardi aendelee kubaki PSG

    Jibu

    Icardi anastahili ongera kwa ofa ya mkataba mrefu

    Jibu

    Icardi anajua mpira

    Jibu

    Akibaki psg watatisha Sana msimu ujao.

    Jibu

    Kwa kocha mwelev uwez kumluhusu atoke kwa kipind hiki

    Jibu

    Abaki hapo hapo

    Jibu

    Abaki hapo hapo👊

    Jibu

    Hongera sana.

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.