"Itakuwa Heshima Kuwa na Salah Bayern"

Mkurugenzi mkuu wa Bayern Munich Karl-Heinz Rummenigge amebainisha kuwa itakuwa “heshima” kumsajili mshambuliaji wa Liverpool Mohamed Salah lakini anasema kuwa hawana mpango wowote wa kumleta Ujerumani.

Salah, ambaye alijiunga na Liverpool kutoka Roma ya Italia mnamo 2017, amekuwa bora zaidi chini ya Jurgen Klopp na kuwa mmoja wa washambuliaji bora ulimwenguni, licha ya kushindwa kufanikiwa Chelsea mapema mwanzoni mwa soka lake.

"Itakuwa Heshima Kuwa na Salah Bayern"

Uchezaji wa Mmisri huyo umevivutia vilabu vingi vikubwa barani Ulaya huku Rummenigge akimtazama nyota huyu mwenye umri wa miaka 28, akimlinganisha na wachezaji kama Lionel Messi na Cristiano Ronaldo, hata hivyo hatarajii Salah kuwasili katika kilabu cha Bundesliga wakati wowote hivi karibuni.

“Kwa maoni yangu, Salah ndiye Messi wa Afrika na kwa kweli ana ujuzi wa kucheza kwa timu bora ulimwenguni,” Rummenigge alizungumza na ON Time Sports.

“Alichofanikiwa kinaweza kulinganishwa na kile ambacho Messi na Ronaldo walifanya na Barcelona na Real Madrid.

“Kwa sasa hatuna mpango wa kumsaini Salah, lakini kwa kweli itakuwa heshima kuwa naye.”

Nyota huyo kwa sasa ndiye mfungaji bora wa Ligi Kuu, akicheka na nyavu mara 16 katika mechi zake 22 hadi sasa kwenye kampeni ya msimu huu.


TENGENEZA MKWANJA UKIWA NA MERIDIANBET 

Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye  kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.

SOMA ZAIDI

13 Komentara

    Sallah ni kiungo mzuri sana

    Jibu

    Liverpool wakimuachia Salah watakuwa wamevurugwa sana

    Jibu

    Salah ni mshambuliaji mahiri kwa sasa ndani ya kikosi cha Liverpool,sidhani kama anaweza kupata mafanikio mahali pengine

    Jibu

    Dallas Yuko vizuri

    Jibu

    Salah baba lao

    Jibu

    Kwenye kuhama liver hapo mbona kama kipengele

    Jibu

    Sidhani kama liverpool watakubali kumuachia jembe salah

    Jibu

    Dallas Yuko poa

    Jibu

    Salah yuko vizuri

    Jibu

    Salah baki nyumbani kumenoga

    Jibu

    Salah yupo vizuri

    Jibu

    Salah bado

    Jibu

    Salah mwenyew kama Messi full mashauzi

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.