Kwa mujibu wa mgombea uraisi wa Barcelona Joan Laporta, staa wa klabu hiyo Lionel Messi anahitaji zaidi mapenzi kutoka kwa timu na mashabiki na kushinda mataji na sio pesa.
Pesi amekuwa akihusishwa zaidi na kuhamia mabingwa wa Ligue 1, Paris Saint Germain na miamaba ya Ligi Kuu Uingereza Manchester City, tangia alipojaribu kuwasilisha ombi lake la uhamisho mwaka jana.
Sakata la hatma ya Messi na Barcelona linaendelea kuwa kitendawili, ambacho kinaweza kujibika pale Messi atakapofanya maamuzi ya hatma yake.
Hata hivyo, kwa mujibu Joan Laporta, ambaye anagombea Uraisi wa klabu hiyo, anasema kuwa Messi hahitaji kabisa hamasa ya pesa, isipokuwa ni kupendwa na kushinda mataji.
Laporta ameitaja kuwa historia ya mapenzi ya Mesii kwa Barcelona ni historia nzuri sana na kwa mtazamo wake hiyo ndiyo ilipaswa kupaliliwa ili kumpa hamasa zaidi nyota huyo zaidi ya kufikiria kuwa pesa nidyo inaweza kumbadilisha.
“Anatakiwa kupendwa. Anastahili hilo. Na anahitaji kuthaminiwa kwa ofa bora ya kiuchumi ambayo itamfanya aione thamani yake, lakini haendeshwi na pesa.”
Laporta, ambaye anasema anamfahamu vyema Messi na wana uhusiano mzuri, anaamini kuwa atapata nafasi ya kufanya kila awezalo kumshawishi Messi kusalia Barcelona.
“Ni mshindi. Anachohitaji ni kushinda tena na Barcelona. Nitaenda kufanya kila niwezalo kumbakiza hapa.”
Treasure Heroes inakupa nafasi ya kupambania ushindi wako mkubwa kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet! Usisubiri hii, jiunge sasa kufurahia ushindi!
Anaongea kweli kabisa
Messi amekuwa kizungumuzuti ndani ya Barcelona. Kuna haja Barcelona kuachana na Messi na kuendelea na maisha yao.
Barca wanamgangania wenyewe messi atawauza sana tu kwenye mechi
Messi sio poa
Messi afanye maamuzi..
Nice update
Kweli kabisa
Wala ujakosea
Sawa kabisa
Yuko sahihi kabisa
Vizuri tuuuu Kama kwanja mzito ainashida
Messi huwaga anamsimamo sana
Mess muda umeishabarca