Nyota Joao Felix anasema kuwa yeye anataka kuwa kama Antoine Griezmann chini ya Diego Simeone. Staa huyu anasema yeye hana tatizo na staili ya Simeone pale Atletico Madrid.
Atletico walitumia Euro milioni 120 kukamilisha usajili wa kuvunja rekodi yao ya usajili kuinasa saini ya staa huyu baada ya Griezemann kutimkia Barcelona msimu wa joto uliopita.
Hii ilimfanya Felix kuwa mchezaji wa gharama zaidi kwenye historia ya usajili wa klabu, baada ya kufanikiwa kuwapita baadhi ya klabu kadhaa zilizokuwa zikiiwania saini yake pia.
Mwanzo wake haujawa mzuri sana pale Atletico Madrid, akiwa amefanikiwa kupata magoli 8 tu na kutoa pasi za usaidizi tatu katika mechi 35 alizocheza kwa michuano yote. Licha ya kusumbuliwa na majeraha, anaamini anweza kuwa bora kama Griezmann klabuni hapo.
Simeone anaamini kuwa staa huyu ataendelea kuwa bora zaidi kadri anavyoendelea kukomaa katika soka. Na anatarajiwa kuwa ataweza kuziba pengo la Griezmann.
“Kama nikiweza kufanya kile alichokifanya Griezmann au kuboesha zaidi, itakuwa poa kwa kuwa ameweza kujijengea historia kubwa na klabu” -Joao Felix
Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.
Njiku
Mafanikio hayagi kiurahisi ila anachotakiwa ni kukataa buti na atakuwa kuja kama grizman na hata kuwa na mafanikio kumpita huyo grizman
Sylvester
Joao Felix ni kweli ana ndoto nyingi sana pale Atletico na nina imani atafanikisha kwani bado ana umri mdogo na ni mtaalamu sana kwenye mpira
Shafii
Unapokua unataka kutimiza ndoto ambayo unayo sio jambo rahisi Sana ila cha msingi ni kupambana na nidhamu ya hali ya juu.
Sadick
Imekuwa kawaida mchezaji muhimu anapoondoa timu husika hukimbilia kutafuta mbadala kwa kuamini atafanya vizuri kama mtangulizi wake jambo ambalo huwa si rahisi. Inaweza kuchukua muda kwa Joao Felix kuziba pengo la Griezmann#meridianbettz
Ester jackson
Sikuzote ukitaka mafanikio lazima uangalie pale unapotaka kufika au zaidi na pia ujitahidi sana na kuwa na tamaa ya kufikisha malengo yako
Zeiyana
Joao Felix hamekua na matokeo mabovu toka haende atletico Madrid akiendelea na matokeo hayo sijui kama hataweza kufikia hayo malengo yake
Adelta
Ni Jambo zuri kua na ndoto za kuja kua mchezaji mkubwa Ila nidhamu katika career yako na kujituma kwa juhudi zote mafanikio yatakuja na ndoto zako zitatimia.
Rehema
Hii makala imetulia
Zuhura omary kindamba
Asante kwa taarifa Meridianbet
Saupha mohamed
Makala imetulia mnoo
Neema
Akiamua hatuna kinachoshindikana
Povel
Inawezekana kikubw juhud, bidii, jitihada na maarifa kila kitu kinawezekana hapo
Sauda
Makala safi sana
Mwajumah
Asante kwa taarifa#Meridianbettz
Salma ngende
Vizuri
aisha
Joao felix unachotakiwa ni kufanya jitihada za kutosha ili utimize ndoto zako hakunakinachoshindikana kwenye hii dunia kila kitu kinawezekana tunakutakia kila la kheri na mafanikio mema
Leonard
Apambane tu atafikia anapopataka
Theonestina
Akiwa na Nia inawezekana
felister
ataweza sababu kadri siku zinavyoenda ndo anazidi kukomaa kwenye soka
Dorophina
Cha msingi Ni kukomaa na anachokitaka mpaka akipate asikate tamaa
Caroline
Ni Jambo zuri sanaa
Nasra
Kufikia ndoto unazozihitaji Ni Jambo zuri Sana Ila Cha msingi Ni kujituma kwa dhati na nidhamu ya Hali ya juu.
Devotha
Apende Sana kazi yake awe na atatimiza ndoto zake
Fatuma kasomo
Jambo zuri
Tatu
Kila kitu kinawezekana akijiwekea malengo
Gabriel
Kiukwel dogo anajua sana joao Felix Kama atapata timu yenye kocha mzur ambaye ataitambua nafas yake joao n bonge la mchezaj
Sabrina
Joao Felix ajipange tu kikubwa kujituma na kutazamia msimamo wake asikate tamaa mpaka kufikia malengo lazima atakutana na vikwazo ajikaze tu atamfikia Griezmann
Hope mwaikuka
Nic news
Mariam mtandama
Makala mazur
Rose kapinga
Akaze buti juhudi na maarifa ndio msingi imara wa kupata mafanikio thabiti!!!
Fatina mfingi
Nice news
Ernest
Joao Felix Ameanza vizuri sana safari yake ya soka kama ataongeza juhudi zaidi basi anaweza akawa zaidi ya Griezmann
Furahav
Haya sasa felix kazi kwako.
magdalena
felix yupo vizuri tu asikate tamaa atafika mbali sana changamoto muhimu sana katika kuyafikia mafanikio
David Pere
Joao Felix ni kweli ana ndoto nyingi sana pale Atletico na nina imani atafanikisha kwani bado ana umri mdogo na ni mtaalamu sana kwenye mpira
warda
Ajibebe tu Atafanikiwa