Joshua Zirkzee Atambulishwa Rasmi United

Aliyekua mshambuliaji wa klabu ya Bologna ya nchini Italia Joshua Zirkzee ametambulishwa rasmi ndani ya kikosi cha Manchester United mapema leo baada ya kukamilisha taratibu zote.

Joshua Zirkzee anajiunga na Man United kutokea klabu ya Bologna kwa ada ya uhamisho ya Euro milioni 42 ambazo inaelezwa zitalipwa ndani ya miaka mitatu, Huku Bayern Munich nao wakipata aslimia 50% ya mauzo ya mchezaji huyo kutokana na kipengele walichokieka wakati wanamuuza Bologna.joshua zirkzeeMshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi anakwenda kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji ya Man United akiungana na wachezaji kama Marcus Rashford, Rasmus Hojlund, Alejandro Garnacho ambao watasimamiwa kwa karibu na aliyekua mshambuliaji matata klabuni hapo Ruud Van Nistelrooy kuhakikisha wanafunga mabao ya kutosha ndani ya klabu hiyo.

Mchezaji huyo dili lake lilikamilika siku ya Alhamisi na kusafiri ijumaa nchini Uingereza ambapo jana Jumamosi alifanikiwa kukamilisha vipimo vya afya ndani ya timu hiyo, Huku akisaini mkataba wa miaka mitano mapema leo  huku kukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja.joshua zirkzee

 

 

Mshambuliaji Joshua Zirkzee amezungumza kidogo baada ya utambulisho wake na kusema haya “

Baada ya kuwa na mazungumzo na meneja na viongozi wa klabu, najua jinsi ya kusisimua siku zijazo zitakavyokuwa hapa na siwezi kusubiri kuchukua sehemu yangu katika kufanikisha mafanikio kwa Manchester United.”

“Mimi ni mchezaji ambaye daima amejitolea kila kitu kwa ajili ya kushinda.”

Acha ujumbe