Aliyekuwa kocha mkuu wa Liverpool Jurgen Klopp amesema kuwa Konrad Laimer alikuwa ni moja ya wachezaji ambao alikuwa anawahitaji klabuni kwake .
.Mwaka 2021, Bayern Munich ilifanya usajili wa aliyekuwa kocha wa RB Leipzig, Julian Nagelsmann, kwa ada ya rekodi, na miezi michache baadaye klabu hiyo ikamsajili nahodha wa Leipzig, Marcel Sabitzer.

Baadaye mwaka 2023, Bayern ilifanya tena uhamisho mwingine ndani ya safu ya kiungo ya Leipzig na kumnunua Konrad Laimer. Wakati huo, ununuzi wa kiungo mwingine kutoka Red Bull ulionekana kama uamuzi wa kutatanisha, huku Ryan Gravenberch akipata muda mdogo wa kucheza na Sabitzer akiwa tayari amepelekwa kwa mkopo.
Hata hivyo, usajili huu ulifanyika kwa ombi la Nagelsmann mwenyewe ambaye alihitaji mchezaji wa aina hiyo. Nagelsmann alihitaji mchezaji mwenye uwezo wa kiulinzi kucheza karibu na Joshua Kimmich.
Alimuhitaji mtu mwenye uwezo wa kufanya pressing kali, kurudisha mipira na kwa ujumla kucheza kama kiungo mkabaji (destroyer). Sabitzer wala Gravenberch hawakuwa na sifa hizo. Sabitzer alikuwa kiungo wa kushambulia zaidi (#8) anayesogea mbele kuliko alivyohitaji Nagelsmann, na Gravenberch alikuwa zaidi mchezaji wa kubeba mpira.
Uhamisho huo ulifanikiwa kwa Bayern kwa namna ambayo hawakuitegemea. Laimer alikuja kama kiungo wa kati lakini sasa ni beki wa kulia wa kwanza kikosini. Mabadiliko haya yalitokana na ulazima Benjamin Pavard alihamia Inter Milan, huku Noussair Mazraoui na Bouna Sarr wakiwa majeruhi.



