Jürgen Klopp Afichua Alijaribu Kumsajili Konrad Laimer Kabla ya Kuhamia Bayern Munich

Aliyekuwa kocha mkuu wa Liverpool Jurgen Klopp amesema kuwa Konrad Laimer alikuwa ni moja ya wachezaji ambao alikuwa anawahitaji klabuni kwake .

.Mwaka 2021, Bayern Munich ilifanya usajili wa aliyekuwa kocha wa RB Leipzig, Julian Nagelsmann, kwa ada ya rekodi, na miezi michache baadaye klabu hiyo ikamsajili nahodha wa Leipzig, Marcel Sabitzer.

Jürgen Klopp Afichua Alijaribu Kumsajili Konrad Laimer Kabla ya Kuhamia Bayern Munich

Baadaye mwaka 2023, Bayern ilifanya tena uhamisho mwingine ndani ya safu ya kiungo ya Leipzig na kumnunua Konrad Laimer. Wakati huo, ununuzi wa kiungo mwingine kutoka Red Bull ulionekana kama uamuzi wa kutatanisha, huku Ryan Gravenberch akipata muda mdogo wa kucheza na Sabitzer akiwa tayari amepelekwa kwa mkopo.

Hata hivyo, usajili huu ulifanyika kwa ombi la Nagelsmann mwenyewe ambaye alihitaji mchezaji wa aina hiyo. Nagelsmann alihitaji mchezaji mwenye uwezo wa kiulinzi kucheza karibu na Joshua Kimmich.

Alimuhitaji mtu mwenye uwezo wa kufanya pressing kali, kurudisha mipira na kwa ujumla kucheza kama kiungo mkabaji (destroyer). Sabitzer wala Gravenberch hawakuwa na sifa hizo. Sabitzer alikuwa kiungo wa kushambulia zaidi (#8) anayesogea mbele kuliko alivyohitaji Nagelsmann, na Gravenberch alikuwa zaidi mchezaji wa kubeba mpira.

Uhamisho huo ulifanikiwa kwa Bayern kwa namna ambayo hawakuitegemea. Laimer alikuja kama kiungo wa kati lakini sasa ni beki wa kulia wa kwanza kikosini. Mabadiliko haya yalitokana na ulazima  Benjamin Pavard alihamia Inter Milan, huku Noussair Mazraoui na Bouna Sarr wakiwa majeruhi.

Jürgen Klopp Afichua Alijaribu Kumsajili Konrad Laimer Kabla ya Kuhamia Bayern Munich

Katika hali hiyo, Thomas Tuchel alimtumia Laimer kama beki wa pembeni. Hata hivyo, ni Vincent Kompany ambaye aligundua nguvu na uwezo wake, na hivyo ushirikiano wa Laimer na Olise ukazaliwa.

Hivi karibuni, Jürgen Klopp alifichua kwamba alijaribu kumsajili Konrad Laimer kwa ajili ya Liverpool. Klopp sasa ni mchambuzi wa Magenta TV, akizungumzia Kombe la Dunia pamoja na Thomas Müller. Kocha huyo wa zamani wa Liverpool alikuwa akizungumzia nafasi za Laimer katika timu ya taifa ya Austria.

“Kwa Laimer naweza kusema hivi: ningemchezesha kama kiungo mkabaji. Nilitaka kumleta Liverpool acheze nafasi ya namba 6. Lakini akaenda Bayern,” alisema Klopp.

Kwa kuzingatia mazingira aliyokuja nayo Bayern na mashaka yaliyokuwepo kuhusu usajili wa kiungo kutoka Leipzig, sasa ni wazi kuwa uamuzi huo ulifanikiwa. Na kwa mkataba wake wa muda mrefu na Bayern, ni wazi mambo yameenda vizuri zaidi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.