Ripoti zinasema kuwa klabu ya Juventus wamekataa nafasi ya kumrejesha mshambuliaji wa Barcelona Arturo Vidal katika dili la mabadilishano na Miralem Pjanic.
Kwa mujibu wa Calciomercato, Barcelona walikuwa wanataka kubadilishana wachezaji na Juventus, na walimtoa Vidal ili kumpata Pjanic.
Nyota huyu mwenye miaka 32, alikuwepo Juventus na kufurahia misimu yake minne kati ya mwaka 2011 na 2015. Alishinda taji la ligi na kufikia fainali za Ligi ya Mabingwa akiwa na Juve.
Aliondoka Juventus Julai 2015 na kujiunga na kwenda Bayern Munich, na mwaka 2018 akajiunga na Barcelona. Mkataba wake wa sasa na Barcelona unaisha mwaka 2021.
Hata hivyo, Juve hawajaweza kukubali kurejea kwake, na ripoti zinataja kuwa hiki Kibibi Kizee cha Italia kinaweza kumuachia Pjanic kwa Arthur Melo tu.
Lakini mpaka sasa Arthur hana mpango kabisa wa kuondoka Camp Nou na anadaiwa kuwa hataki hata kubadilisha msimamo wake juu ya hilo. Hataki kabisa kusikia hadithi za kwenda mbali na Messi, anataka kusalia LaLiga.
Daniel
Great player #Meridianbettz
Leonard
mambo ni moto
Isaya massawe
Abakie tu noucamp
Ernest
Pjanic anaweza kusaidia Barca
Zeiyana iddi
Abaki tu na messi uko uko unaweza kujifunza kitu kupitia yeye..!
Gabriel
Ata Vidal anamchango mkubwa sana barca
Mwanaidi
Wamchukue tuu ni mchezaji mahiri sana
mwakalosi
Umri umeshakwenda na kiwango kimepungua
Elika
Abaki tu hapo
Asia Abdy
Ni vyema akibaki
Furahav
Baki tu hapo.
Salma
Afanye maamuzi sahihi
Ester
Kazi na umri apumzike sasa
Rehema
Ni vzr akibaki hapo hapo
David pere
Ashakua mzee huyu jamaa
Dorophina
Umri wake umeenda sana sidhani km ataweza kutoa msaada ipasavyo akienda barca
Mwajuma
Bora abaki tu umri wenyewe ushamtupa mkono
Genia Sikaluzwe
Aendele kubaki tu hapo
sylvester
Arturo vidal miaka ishaenda soka linamuaga mkono sasa huwezi mlinganisha na huyo dogo ambae bado umri unaruhusu
Lombo
meridianbet hamjawai kuboa
Tahiya
Vidal ni mkongwe mpambanaji anajituma sana hawapo uwanjani
Theckla
Amalizie tu Mana kazi na umri
Hamidu
Vidal kwa juve hapana.! Umri ushaenda.
Aziza mushi
Bora abaki tu,maana umri umeenda Sana.
aisha
Umri umeshaenda huyo jamaa
frank patrick
Sasa hivi Juve wadeal na vijana sasa hawa wazee warudi kucheza kwenye league za mataifa yao huko au waende China kukuza league ya kule
Rehema Dickson
Vilad umri ushaenda awezi kulingana na dogo ambae damu inachemka
Emmy cleopa
Bora habaki tu
Neema juma
Sio mbaya akibakii
Povel
Abaki nou camp thanks meridian bet
Amani
Atulize boli tu aende china
Swai
Abaki tu Barcelona
Mariam mtandama
Sio mbaya akibaki
felister
ng’ombe hazeeki maini wamsajili tu
Neema hassan
Bora abaki barcelona
Khadija
umri ushaenda huyo jamaa
Magdalena
Kashazeeka uyo akamalizie uzee katika leage za mataifa
Mwanahamisi
Abaki tuu hapo hapo
SADICK
Akufukuzae hakwambia toka. Vidal atafute malisho pahali pengine #Meridianbettz
Shafii
Vidal kwa Sasa kiwango kishaisha na umri ushamtupa mkono
Lydia Emmanuel Magoti
Bora habaki tuu
Samira
Umri umeshaenda sana
Hidaya Mohammed
Kazi na umri abaki tu hapohapo
Antony Luseno
Arturo kiwango kimeshuka sana
Hope mwaikuka
Bak tu hakuna namna
Samiah
Uzee mwisho chalinze hivyo abaki2
Agness
Abaki tuu
winfrida
kila kitu kina mwanzo na mwisho awaachie vijana sasa
Carolyne
Atapata Pengine