Gazeti la Tuttosport laripoti kuwa beki wa zamani wa kulia wa Real Madrid, Lucas Vázquez, amependekezwa kwa Juventus, huku Alberto Costa akiwa hatoi presha ya kuondoka, lakini Bianconeri wako tayari kupokea ofa ya kati ya €18m-€20m.

Juventus wanahitaji wing-back mpya upande wa kulia na wamepata pendekezo la kumsajili beki wa zamani wa Real Madrid, Lucas Vázquez, ambaye kwa sasa ni mchezaji huru baada ya mkataba wake kumalizika kwenye klabu ya Bernabéu.
Kulingana na Tuttosport, kikwazo kikuu ni mshahara wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34, ambaye alipokea €4.5m katika msimu wake wa mwisho akiwa Real Madrid.
Hata hivyo, mkurugenzi wa Juve, Damien Comolli, atajadili uwezekano wa kumsajili Vázquez pamoja na kocha Igor Tudor, ingawa hadi sasa Mspaniola huyo si chaguo la haraka kwa klabu hiyo.
Malengo mengine ya Juve upande wa kulia ni pamoja na Dodo wa Fiorentina, ambaye thamani yake ni €30m, na Josha Vagnoman wa VfB Stuttgart.



