Juventus Yaanza Kumpigia Rada Lucas Vazquez

Gazeti la Tuttosport laripoti kuwa beki wa zamani wa kulia wa Real Madrid, Lucas Vázquez, amependekezwa kwa Juventus, huku Alberto Costa akiwa hatoi presha ya kuondoka, lakini Bianconeri wako tayari kupokea ofa ya kati ya €18m-€20m.

Juventus Yaanza Kumpigia Rada Lucas Vazquez

Juventus wanahitaji wing-back mpya upande wa kulia na wamepata pendekezo la kumsajili beki wa zamani wa Real Madrid, Lucas Vázquez, ambaye kwa sasa ni mchezaji huru baada ya mkataba wake kumalizika kwenye klabu ya Bernabéu.

Kulingana na Tuttosport, kikwazo kikuu ni mshahara wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34, ambaye alipokea €4.5m katika msimu wake wa mwisho akiwa Real Madrid.

Hata hivyo, mkurugenzi wa Juve, Damien Comolli, atajadili uwezekano wa kumsajili Vázquez pamoja na kocha Igor Tudor, ingawa hadi sasa Mspaniola huyo si chaguo la haraka kwa klabu hiyo.

Malengo mengine ya Juve upande wa kulia ni pamoja na Dodo wa Fiorentina, ambaye thamani yake ni €30m, na Josha Vagnoman wa VfB Stuttgart.

Juventus Yaanza Kumpigia Rada Lucas Vazquez

Juventus wanaendelea na mazungumzo na Sporting CP kuhusu Alberto Costa. Mreno huyo alijiunga na Bibi Kizee Januari iliyopita, na kocha Igor Tudor anataka aendelee kuwepo katika uwanja wa Allianz. Hata hivyo, Juventus wapo tayari kumuuza Costa kwa dau la €18m hadi €20m, iwapo ofa nzuri itawasilishwa.

Kwa upande mwingine, Timothy Weah tayari amekubaliana masharti binafsi na Marseille ya Roberto De Zerbi, na sasa Marseille wako kwenye mazungumzo na Bibi Kizee kuhusu ada ya uhamisho wa mchezaji huyo wa kimataifa wa Marekani (USMNT).

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.