Gwiji wa Bayern Munich – Oliver Kahn amesifu kiwango cha Serge Gnabry baada ya kung’ara kwenye Mashindando ya Ligi ya Mabingwa – UEFA msimu huu.
Gnabry ambaye mpaka sasa anajumla ya magoli 9, amekuwa kwenye kiwango thabiti msimu huu akicheza katika nafasi ya winga. Katika mchezo wa nusu fainali dhidi ya Lyon, Gnabry alifunga magoli mawili kati ya matatu yaliwapeleka Bayern hatua ya fainali na sasa, Bayern Munich atamenyana na PSG.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kahn amesema ” magoli yake ni ya kiwango cha dunia. Ni mchezaji aliyeongezeka kiwango kwa miezi kadhaa iliyopita. Grafu yake inapanda kila mwaka. Yupo mbali kufikia kiwango cha dunia lakini ni mchezaji mzuri, anamchezo mzuri.

“Lakini pia kocha anahusika, mawasiliano ya kocha. Hiyo ni sifa mojawapo ya Hansi [Flick]. Anaweza kushughulika na wachezaji wa aina mbalimbali, mara zote ana maneno sahihi ya kuzungumza. Hiyo inatuletea mafaniko kwa sasa.
Kahn awapongeza pia wachezaji wenye uzoefu.
“Nimelinganisha vitu vingi sana kwa uzoefu wangu. Kwa namna ambavyo hawa wachezaji wanawaza magoli, ni jambo la kuvutia. Wanataka kushinda Ligi ya Mabingwa,watafanya lolote kwa ajili hiyo lakini unatakiwa kuwa na muongozo.
“Tunae Manuel Neuer kama nahodha anayeweza kuwaongoza wachezaji wengine. Thomas Muller pia amekuwa mfano wa kuigwa na wengine, anazungumza sana. Joshua Kimmich anamorali sana, anafanya kila kitu kwaajili ya maendeleo.
“Kitu cha kipekee ni kwamba, wengi wao wameshashinda kila kitu lakini bado hawachoki.”
Bayern Munich hawajapoteza mchezo wowote 2020 wakiwa tayari wamecheza michezo 20. Ushindi dhidi ya PSG utakamilisha jumla ya mataji 3 kwa Bayern Munich msimu huu.
Drops and Wins!
Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.


Devotha
Gnabry anakiwango kizuri sana hata hivo safu ya ushambuliaji Bayern imejitosheleza wapo vizuri sana
farida ahmadi
Habari njema Sana
Gabriel
Flick ni kocha mzur na kaul ambayo alioongea kahn yuko sahihi kabisa
Povel
Gnarby amekuwah mcharo kwl mmoja wa wachezaj walionyesha kiwango cha Hal ya juu ue
Amiri Kayera
Ni kwer kwasasa uwez wake unaongezek
Sabrina
Kijana yuko Fiti
Theonestina
Jamaa Yuko vizur
Janeflora malisa
Yupo kiwango
David Pere
Kitu cha kipekee ni kwamba, wengi wao wameshashinda kila kitu lakini bado hawachoki.”
Fatuma kasomo
Yupo vizuri
Mwanahamisi
Jamaa Yuko vizuri
Shan
Yuko vizur sana!
Ernest
Kusema ukweli kocha anastahili pongezi zake kwa kumfanya Gnabry Ang’ae sana si tuu ndani ya UEFA bali ata kwenye ligi
warda
Ni kweli kabisa Flick amehusika sana#Meridianbettz
Sauda
Gnabry yupo vizuri sana
Nasra
Yuko vzuri
Ester jackson
Good job koch
rama
Maoni:vizuri sana inabidii aongezee juhudi sasa
Dorophina
Gnabry yupo vizuri kiwango chake cha kimataifa hasa kwenye safu ya ushambuliaji
Mwajumah
Ni kweli kwa sasa uwezo wake umeongezeka#Meridianbettz
Khadija
Good job koch#meridianbettz
felister
ni kweli kwa sasa hivi kiwango change kimeongezeka
Adelta
Habari njema Sana
@meridianbettz
Magdalena
kocha yuko vizuri sana kazi ameifanya ya ziada
Zeiyana
Kiukweli bado Bayern munch wana kikosi kizuri na ndio mabingwa wetu msimu hii asilimia mia PSG wajipange sana hawana mbio za kuwafikia bayrne hata waluke
Fatina mfingi
Jamaa bad yupo moto
Lydia Emmanuel Magoti
Kijana yupo vizuri kwa Sasa kiwango chake kimezidi kuwa juu
Tatu
Gnarby ni mchezaji anayejituma sana lazima kiwangi chake kipande
Samira
Ameng’aa sana kipindi kifupi kuanzia kwenye uefa hadi ligi
Samiah
Yupo vzr
Hope mwaikuka
Namkubal
Furahav
Namkubali.
Issa
Munich msimu wenu huu
Shafii
Kweli maisha yanabadilika arsenal walimuona Kama sio msaada kwao sasa dogo amekua gumzo ulimwenguni.
Omary lukumbi
Kijana yuko fit na amekua kwenye kiwango kizr sana
aisha
Ni sahihi jamaa kiwango chake kimekngezeka