Klopp : Kumfunga City Sio Kutwaa Ubingwa.

Meneja wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema ushindi dhidi ya Manchester City siku ya Jumapili katika mchezo wa ligi kuu haumaanishi kwamba watatwaa ubingwa huo msimu huu.

 

Liverpool wanashika nafasi ya pili nyuma ya Manchester City kwa alama moja pekee wakati wakielekea katika dimba la Etihad kuvaana na wananchi siku ya Jumapili baada ya kutoka sare ya 2-2 katika mchezo wao wa kwanza pale Anfield.

“Kama tutashinda dhidi ya City, ambayo ni vigumu, sidhani kama kuna mtu atafikiri, ubingwa umesha amuliwa, kutokana na ubora wa mpinzani wetu” Klopp alisema baada ya ushindi hapo jana.

“Tunaenda kucheza dhidi ya timu bora kwa sasa duniani, lakini tutajaribu. Tulichokianza kwa miezi michache iliyopita, tumetengeneza msingi.

Klopp ameongoza Liverpool kucheza robo fainali ya Ligi ya mabingwa, nusu fainali ya kombe la FA na kutwaa ubingwa wa Carabao msimu huu.


3500 NI YAKO UKIJIUNGA TU MERIDIANBET!

Una nafasi ya kupata bonasi ya shilingi 3500 kwa ajili ya kuanza safari yako ya kasino ya mtandaoni ya Meridianbet.

Kubeti Poa - Bonasi Kubwa

Jisajili sasa

Acha ujumbe