Mfungaji anayeongoza kwa wakati wote wa Ujerumani, Miroslav Klose ameteuliwa kuwa Kocha msaidizi wa Mabingwa wa Ujerumani, Bayern Munich kwa msimu ujao.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 41 amekuwa mkufunzi wa vijana kwenye Klabu hiyo kwa miaka miwili iliyopita baada ya kustaafu kama mchezaji mnamo 2016.
Alitumia misimu minne kama mchezaji wa Bayern kutoka 2007, akishinda ligi na vikombe vingine. Kocha mkuu wa Bayern, Hansi Flick, aliyetia saini kuwaongoza Miamba hao mwezi uliopita, alikuwa kocha msaidizi wa Ujerumani wakati Klose anaongoza mashambulizi kama Mchezaji kwenye Ubingwa wao wa Kombe la Dunia la 2014.
Klose alifunga mabao 71 katika michezo 137 kwa Ujerumani kati ya 2001 na 2014. Alicheza pia kwa Kaiserslautern, Werder Bremen na klabu ya Italia, Lazio.
Klose anajulikana sana kwa uchezaji wake bora na timu ya taifa ya Ujerumani. Alikuwa sehemu ya kikosi cha Ujerumani kilishinda Kombe la Dunia la 2014, hapo awali kilimaliza nafasi ya pili (2002) na ya tatu (2006, 2010) kwenye mashindano, na Kupoteza Fainali katika UEFA Euro 2008 na nafasi ya tatu katika UEFA Euro 2012.
Antony Luseno
Mchangako wako natumai utazaa matunda
Adelta
Mchango wake utazaa matunda
Neema juma
Klose anajulikana sana kwa uchezaji wake bora. Yuko vzr sana.
tahiya
yuko vizur sana
johnm
ni mwanzo mzuri kwake kuwa kocha
Zainabu
Tunamkaribisha kocha mpya tunaitaji kazi nzuri
Njiku
Jamaa alikuwa vizuri sanaa
Neema hassan
Hongera kwake..
felister
karibu Bayern natumai hatoiangusha timu
aisha
yuko vizuri sana taleta matunda
Gabriel
Yuko vizur
JULIANA
Yuko vizuri
Shafii
Jamaa alikua fundi Sanaa
Mwajuma
Namkubali sana
mathayo sonje
ni jambo jema kwa close maana anaandaa mazingira ambayo yatamfanya awe bora kama walivyo wakima zizu
Mariam
Yupo vizur
Geniaskaluzwe8
Yuko vizuri sana
SADICK
Mzee wa magoli ya vichwa. Asante meridian kutujuza mambo motomoto yanayoendelea ulimwenguni
Ernest Kimeru
All the Best Klose on your new career.
Povel liwongolo
Ni Jambo la kheri kwa uongozi wa miamba ya soka la ujerumani kuheshimu na kumdhamini mchango wake aliotowak katika miamba hyo mm namtakiah mafanikio katika majukumu mapya ya kazi
Dorophina
Atasaidia kuiinua zaidi bayern munich
winfrida
bonge la dili
Ester jackson
Yuko vizuri sana apige kazi tu
Christopher
Huyu jamaa analijua vizuri soka la ujerumani kuanzia ngazi ya vilabu mpaka timu ya taiga, kwahyo naona uwepo wake unaweza kuongeza kitu pale Bayern munich
Mwanaidi
Ni mtu muhimu sana huyo Bayern munich
David pere
Jamaa anafaa Sana kumsaidia
Rehema Dickson
Tunamkaribisha kocha mpya tunaitaji kazi nzuri
Furahav
Safi