Imeripotiwa kutokea huko THE HAGUE, Netherlands kuwa kocha mkuu wa kikosi cha timu ya taifa Dutch, Ronald Koeman alihitaji matibabu zaidi na kukimbizwa hospitalini kutokana na tatizo la mshtuko wa moyo.
Mke wake alizungumza juu ya hali ya kiafya ya kocha huyo kwa gazeti la De Telegraaf siku ya Jumapili mwishoni mwa wiki iliyopita.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 57 kwa sasa alipatwa na tatizo la ugonjwa wa moyo ambapo akatakiwa kukimbizwa hospitalini huko Amsterdam ikiwa ni mara baada ya kutopata nafuu wakati akiwa nyumbani kwake.
“Alivyowahishwa hospitalini na kwa kuhudumiwa vyema na madaktari tuliowakuta ilisaidia sana hali yake kuendelea kuwa sawa kabisa,” alisema hayo Bartina Koeman.
Koeman, amekuwa na kikosi cha taifa cha Dutch tangu mwaka 2018, na akategemewa kuruhusiwa kwenda nyumbani kutoka hospitalini siku ya leo.
“Ilikuwa ni mshtuko!” Shirikisho la Kandanda la taifa la Uholanzi liliandika hivi kupitia mtandao wao wa Twitter.
“Tunayo furaha, mambo yamekuwa vyema zaidi. Nguvu anazo na kocha huyo anaendelea kupata nafuu zaidi.”

Enzi za ujana wake Koeman, alikuwa akikipiga kwa klabu za Ajax, PSV, Feyenoord na klabu ya soka ya Barcelona pamoja na timu ya taifa kote huko akiwa kama mlinzi. Kwa sasa ameshakiwezesha kikosi chake kufuzu kuingia kwenye michuano ya Euro 2020 akiwa na taifa lake la Uholanzi.
Hata hivyo, michuano imeahirishwa kwa sasa na kusogezwa hadi mwaka 2021 itakapofanyika kama ilivyopangwa mwanzo.


Furahav
Utapona mzee.
Theckla
Atapona tu Mungu ni mkubwa
Salma
Mungu atakusaidia utakuwa poa
Tahiya
Utakuwa salama
Dorophina
Atapona tu pole yake
Hopemwaikux
Inshallah utapona
Amani
Mungu ata mjalia atapona
Zeiyana iddi
Mungu hatamsaidia hatapona
Nasra
Atapona mungu amsaidie tu
felister
mwenyezi mungu ndo muweza wa kila kitu atapona na atarudi ktk hal yk ya kawaida
Lydia Emmanuel Magoti
Mungu atamsaidia atapona
Lombo
atapona2
Neema juma
Atapona tu
mathayo sonje
tunamuombea kwa Mungu apone aendelee na majukumu yake ya kimichezo
Hidaya Mohammed
Mwenyezi mungu atamuafu.
Gabriel
Utampona 🙏
Ananiambtz
Mungu amsaidie apone haraka aendelee na majukumu yake
Winfrida
Pole sana Dutch
Neema hassan
Mungu amponye aendelee na majukumu yake..
Shafii
Mungu amjalie aendelee na majukumu yake
Elika
Hakika utapona.na utarudi kwenye hari yako kama zamaniii