Kocha Wales Atarajia Ramsey Kusalia Timu ya Taifa

Kocha wa timu ya taifa ya Wales Rob Page amesema anatarajia kiungo wa timu ya taifa ya Wales Aaron Ramsey kusalia kwenye timu hiyo baada ya mwenzake Gareth Bale kustaafu.

Gareth Bale ametangaza kustaafu kucheza soka rasmi siku ya jana akiwa na umri wa miaka 33 baada ya kutumikia mpira kwa muda mrefu. Staa huyo ameamua kuachana na mpira kwa ujumla kuanzia ngazi ya klabu mpaka timu ya taifa.KochaKocha wa Wales anaamini kua kiungo wa timu hiyo Aaron Ramsey kusalia katika timu ya taifa ya Wales na kutokufata nyendo za staa mwezake wa timu hiyo Gareth Bale. Kocha huyo anaamini Ramsey aatasalia ndani ya timu hiyo ili kujiandaa na michuano ya kufuzu Euro 2024 itakayoanza mweze Machi mwaka huu.

Kocha huyo anasema anaamini Ramsey mwenye umri wa miaka 32 ana vingi bado vya kujitolea katika timu ya taifa ya Wales, Lakini akisisitiza kua kiungo huyo ni mchezaji mzuri na anaweza bado kujitoa kwenye timu ya taifa ya Wales.KochaKocha Rob Page hakusita kusikitika juu ya kustaafu kwa staa Gareth Bale kwani anaamini bado alikua anamhitaji kwenye timu yake kutokana na uwezo aliokua nao, Lakini Rob Page hakua namna zaidi ya kumpongeza staa huyo kutokana wakati bora zaidi uwanjani.

Acha ujumbe