Kocha wa Barcelona Ronald Koeman amenukuliwa akipingana na raisi wa mpito wa klabu hiyo – Carlos Tusquets baada ya kusema angemuuza Messi majira ya kiangazi.
Siku ya Ijumaa, Tusquets alinukuliwa akitoa maneno hayo ambayo alidai kwa sababu za kiuchumi, majira ya kiangazi yalikuwa sahihi zaidi kumuuza Messi. Kwa Tusquets, ingepunguza fedha nyingi za mshahara pamoja na kuongezea timu mapato.
Kwa Koeman, hii sio sahihi. Akizungumza na waandishi wa habari, kocha huyo amesema ” tunafahamu hali ya Messi. Kama kuna mtu yeyote ambaye anapaswa kuamua hatma yake, basi ni yeye [Lionel Messi] mwenyewe.
“Sijali kinachosemwa nje ya klabu, lakini maneno yanayosemwa ndani ya klabu hayatusaidii kuwa watulivu na kufanya kazi yetu. Hatuwezi kuzuia ya nje ila ya ndani hiyo ni habari nyingine.
“Kama kumuuza Messi majira ya kiangazi ni maoni binafsi ya Tusquets, ninaheshimu hilo, lakini Leo mwaka mmoja kwenye mkataba wake na yeye ndiye atakayefanya maamuzi.”
Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!
Shakila mrope
Asant kwa uchambuzi
Sadick
Waswahili wanasema Lugha gongana. M/kiti ameangalia fedha na Kocha anaangalia mshikamano ktk timu
Khadija
Uchambuzi upo poa
Adelta
Uchambuzi uko vizuri na kocha Yuko sahihi
Lydia Emmanuel Magoti
Duu Sasa bari imegeuka kwaviongozi Messi Sasa kilamtu umzungumzia Mambo yashakuwa juu yamambo
Caroline
Messi wamuache tyu
Sarah
Uchambuzi uko poa
Issa
Mess yupo poa sana
lombo
asante meridianbet kwa habar moto moto
Neema
Nimeielewa hy habarii
Dorophina
Messi kuondoka barca haitowezekana hata
Saupha mohamed
Uchambuzi upo vizuri
Magdalena
Messi ni wa Barcelona
felister
uchambuzi mzuri
Sauda
Makala imetulia.
Tatu
Mess abaki Barcelona
Sabrina
Wamuache tu messi azekee hapo hapo
Janeflora malisa
🔥
aisha
Messi kama messi
warda
Koeman Yupo sahihi