Klabu ya Leicester City ambayo imemfuta kazi aliyekua kocha wake Steve Cooper sasa wamemuajiri aliyekua kocha msaidizi wa klabu ya Manchester United Ruud Van Nistelrooy raia wa kimataifa wa Uholanzi.
Leicester City wamefanya mazungmzo na kocha Van Nistelrooy wiki hii baada ya kumfuta kazi Steve Cooper ambapo mazungumzo yao yalienda vizuri na kupelekea kocha huyo kukubali kuchukua mikoba ya kuinoa timu hiyo ambayo haipo kwenye kipindi kizuri sana ndani ya ligi kuu ya Uingereza.Kocha Ruud Van Nistelrooy ambaye aliiongoza klabu ya Manchester United kwa michezo minne baada ya Erik Ten Hag kufukuzwa kazi na kufanikiwa kushinda michezo mitatu na kusuluhu mchezo mmoja, Hali iliyowafanya mashabiki wa Man United kutamani kumuona akiendelea kua sehemu ya timu hiyo.
Baada ya kocha Ruben Amorim kutangazwa kama kocha mkuu wa klabu ya Manchester United Van Nistelrooy alitimka klabuni hapo, Lakini Leicester City wameonekana kumuamini na kuona ndio kocha sahihi kwasasa kuivusha klabu yao na kuamua kumpa timu na sasa ni muda wa gwiji huyo kuonesha ubora ndani ya kikosi cha mabingwa hao wa Uingereza mwaka 2016.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.