Beki wa kimataifa wa Argentina anayekipiga ndani ya klabu ya Manchester United Lisandro Martinez inaelezwa atakosekana katika mchezo wa leo dhidi ya klabu ya Ipswich Town.
Lisandro Martinez inaelezwa alikua na majeraha madogo ambayo yalimfanya akashindwa kujiunga na timu ya taifa ya Argentina, Hivo majeraha hayo yanaonekana bado hayajapona na ndio sababu atakosekana katika mchezo wa leo ugenini dhidi ya klabu ya Ipswich.
Beki huyo wa kimataifa wa Argentina amekua akiandamwa na majeraha ya mara kwa mara tangu ajiunge na klabu ya Manchester United akitokea klabu ya Ajax mwaka 2022, Hali hiyo imekua ikiiumiza klabu hiyo kwani beki huyo amekua moja ya wachezaji muhimu klabu hapo hivo kukosekana kwake inakua pengo kubwa.
Beki Lisandro Martinez sasa anaongeza orodha ya majeraha klabuni hapo kufikia wawili kwani mchezaji pekee ambaye alikua hajapona klabuni hapo ni Harry Maguire peke, Kuongezeka kwa beki huyo kunafanya idadi kuongezeka kufikia wawili lakini Man United kwasasa wameonekana kua na machaguo ya kutosha kwenye eneo la ulinzi.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.