Liverpool, Chelsea na Man United Wanampigania nyota wa Inter Milan Damfries Kwa Pauni 21M.

Denzel Dumfries anaaminika kuwa na kipengele cha kuachiliwa cha pauni milioni 21, huku Liverpool, Chelsea na Manchester United zikiwa miongoni mwa vilabu vinavyomfuatilia nyota huyo wa Inter Milan.

Liverpool, Chelsea na Man United Wanampigania nyota wa Inter Milan Damfries Kwa Pauni 21M.

Dumfries amekuwa akihusishwa na uhamisho wa kwenda EPL kwa muda mrefu, na inaonekana kuondoka Milan kunaweza kutokea majira haya ya joto.

Inaelezwa kuwa ana kipengele cha kuachiliwa cha pauni milioni 21 kwenye mkataba wake na Inter, jambo lililomfanya kuvutia vilabu kadhaa. Liverpool wanatarajiwa kuimarisha safu yao ya ulinzi majira haya licha ya kutumia pesa nyingi msimu uliopita.

Wachezaji kama Miloš Kerkez, Jeremie Frimpong na Giovanni Leoni walijiunga kutoka AFC Bournemouth, Bayer Leverkusen na Parma.

Hata hivyo, mabingwa watetezi wa ligi wanatafuta kuongeza uzoefu zaidi kwenye safu yao ya nyuma, na Dumfries ni miongoni mwa wachezaji wanaoweza kuwasaidia.

Liverpool, Chelsea na Man United Wanampigania nyota wa Inter Milan Damfries Kwa Pauni 21M.

Liverpool watakumbana na ushindani mkubwa kutoka Chelsea na Manchester United ambao pia wanamuwinda beki huyo anayependa kushambulia.

Chelsea tayari wana chaguo kama Reece James na Malo Gusto upande wa kulia, lakini majeraha ya mara kwa mara ya James yanaweza kuwalazimisha kutafuta mbadala mwingine.

Kwa upande wa United, wanatafuta beki wa kulia wa kuongeza ushindani kwa Diogo Dalot na Noussair Mazraoui.

Kwa kuwa ana kipengele cha kuachiliwa chenye thamani ndogo, vilabu hivi vitakumbana na ushindani mkali wa kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29, ambaye ameanza mechi 11 za ligi msimu huu.

Vilabu vingine kama Manchester City, Tottenham Hotspur na Newcastle United pia vinaonyesha nia, huku pia Saudi Pro League ikimfuatilia kwa karibu.

Liverpool, Chelsea na Man United Wanampigania nyota wa Inter Milan Damfries Kwa Pauni 21M.

Dumfries anatarajiwa kusaidia Inter Milan kurejea kwenye ushindi watakapokutana na AS Roma mwishoni mwa wiki hii baada ya mapumziko ya kimataifa.

Nerazzurri wanaongoza Serie A kwa tofauti ya pointi sita, lakini hawajashinda mechi zao tatu za mwisho, baada ya kupoteza 1-0 dhidi ya AC Milan na kutoka sare dhidi ya Atalanta na Fiorentina.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.