Liverpool wanaripotiwa kuwa na nia ya kuwauza wachezaji wengine watano kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho wa majira ya joto.
Jurgen Klopp ana nia ya kuongeza angalau wachezaji wawili wakubwa katika wiki zijazo akionekana kuimarisha safu yale ya katikati na safu ya ushambuliaji.
Marko Grujic na Taiwo Awoniyi tayari wameruhusiwa kuondoka kwenda Porto na Union Berlin, mikataba ambayo inatarajiwa kuleta takriban pauni milioni 17.
Lakini kwa mujibu wa Liverpool Echo, miamba hawa wa Merseyside wako tayari kupakua wachezaji wengine watano wa kikosi wiki zijazo.
Liverpool inadaiwa itaanza kuzingatia zabuni yoyote muhimu za Nat Phillips, Divock Origi, Harry Wilson, Neco Williams na Xherdan Shaqiri.
Uongozi wa klabu unasemekana unaamini kwamba wanaweza kukusanya kiasi cha £70m kupitia mauzo ya wachezaji hao wote.
Kasino ya Mayan Eagle inakukufanya kuwa bingwa wakati wowote unapoamua kuicheza. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!
Ernest
Jurgen Klopp na Liverpool kwa ujumla wapo katika wakati mgumu sana msimu huu