Liverpool wamefanya mazungumzo kuhusu uwezekano wa kumsajili beki wa kati wa Paris Saint-Germain, Illia Zabarnyi, kwa mujibu wa DaveOCKOP.

Ripoti za awali katika dirisha hili la usajili zilieleza kuwa mawakala wa Zabarnyi walimpendekeza mchezaji huyo kwa Liverpool. Beki huyo wa kimataifa wa Ukraine alijiunga na mabingwa wa Ulaya, Paris Saint-Germain, kutoka Bournemouth majira ya kiangazi yaliyopita, lakini hakupata nafasi ya kucheza mara kwa mara, hasa katika kampeni ya ushindi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Kutokana na hali hiyo, kurejea England, ambako aliwahi kung’ara kwa misimu miwili akiwa Bournemouth, kunaweza kuwa hatua nzuri kwa maendeleo yake.
Sasa inaelezwa kuwa Liverpool wameendelea na mazungumzo kuhusu uwezekano wa kumsajili.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 anatajwa kuwa mmoja wa wachezaji ambao Liverpool wanaweza kufikiria kumsajili baadaye katika dirisha hili la usajili, huku wawakilishi wake wakijaribu tena kumhamishia Anfield.
Kwa sasa Liverpool wanakabiliwa na tatizo kubwa katika safu ya ulinzi, ambapo Virgil van Dijk ndiye pekee aliyebaki akiwa fiti miongoni mwa mabeki wa kati wa kikosi cha kwanza.

Giovanni Leoni, Jérémy Jacquet na Joe Gomez wote wako nje kutokana na majeraha, huku pia mabeki wa kulia Conor Bradley na Jeremie Frimpong wakikosekana.
Kutokana na hali hiyo, Liverpool wamelazimika kuwatumia wachezaji wa kikosi cha vijana katika mechi za maandalizi ya msimu. Hata beki wa kushoto Luke Chambers alicheza kama beki wa kati katika kipigo cha mabao 4-2 dhidi ya Leeds United.
Hata hivyo, mwandishi wa Sky Sports, Mark McAdam, hivi karibuni alifichua kuwa Liver hawana mpango wa kumsajili beki wa kati kabla ya mwisho wa dirisha hili la usajili.
Alisema: “Jibu tunalopewa ni hapana. Kwa uelewa wangu, Liver hawataingia sokoni kumsajili mchezaji katika kipindi cha wiki nne hadi sita zijazo. Watalazimika kuvumilia hali ilivyo kwa sasa, kisha kusubiri wachezaji wao walioumia warejee ili safu ya ulinzi irejee katika nguvu zake kamili.”



