Wachezaji Trent Arnold and Naby Keita walitumiwa maoni ya kibaguzi baada ya mechi kati ya Liverpool dhidi ya Real Madrid. Liverpool wamesema ifike wakati vitendo vya kibaguzi dhidi ya watu weusi kiachwe.
Mchezo wa Real Madrid na Liverpool ulomalizika kwa Madrid kushinda mabao 3-1, huku magoli mawili kati ya hayo yakifungwa kwa mapungufu ya upande wa Trent Anorld.
Mashabiki wengi wamekuwa wakihofia Trent kupoteza kujiamini kwake baada ya kupata korona na kutokuitwa kwa Trent kwenye timu ya taifa ya Uingereza. Trent amekuwa na wakati mgumu sana msimu huu baada ya kupata Korona na kukosa michezo mingi ya Liverpool.
Katika upande wa maoni katika chapisho la Instagram, Naby Keita na Trent Anorld walitumiwa emoji za nyani ambazo moja kwa moja zinahusianishwa na ubaguzi wa rangi.
Katika mahojiano baada ya mechi Klopp alisema kwamba alimtoa Keita kwa sababu hakucheza vizuri kutokana na kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu.
Kumekuwa na jitihada nyingi sana kukemea vitendo vya ubaguzi duniani kote. Ni wakati sahihi sasa kwa wadau wa michezo duniani kote kuzuia vitendo hivi, kwani lengo kuu la michezo nikuendeleza amani na upendo miongoni mwa watu!
INAWEZEKANA KUWA MILIONEA BILA KUVUJA JASHO NA KASINO YA ODD ONE OUT.
Odd One Out kutoka Meridianbet ni moja ya kasino maridhawa yenye picha halisi, ambayo inakupa nafasi ya kushinda kadri uwezavyo na kuwa milionea mara baada ya mzunguko kukamilika.
Adelta
Ubaguzi sio ubinadamu waachane na hizo tabia wachezaji mpira kwani mungu Ndiye muumbaji
neema juma
Ubaguzi sio poa kabisaa
warda
Kwa kweli sio kitu kizuri