Kocha mkuu wa Chelsea Thomas Tuchel amethibitisha kwamba Romelu Lukaku ataukosa mchezo wa marudiano dhidi ya klabu ya Real Madrid katika Ligi ya Mabingwa siku ya Jumanne.

Chelsea ilipoteza kwa 3-1 mchezo wa kwanza katika uwanja wa Stamford Bridge wiki iliyopita ikiwa ni hatua ya robo fainali ya michuano hiyo na Lukaku alikosa nafasi mbili za wazi baada ya kuingia kipindi cha pili.
Lukaku hakucheza katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Southampton siku ya Jumamosi kutokana na majeraha na bado hajapona kuweza kusafiri mpaka jiji la Madrid kwaajili ya mchezo wa Marudiano.
Tuchel alisema: “Callum Hudson-Odoi, Ben Chilwell na Romelu Lukaku hawato safiri.”
“Azpilicueta amepona Covid-19 na atajiunga na kundi lakini Ross Barkley anaumwa.
Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.



