Beki chaguo namba moja la Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck, mechi 11 zote ameanza kikosi cha kwanza ambazo Simba imecheza kwa msimu huu wa 2020/21.
Amefanya makosa matatu yaliyosababisha timu yake kufungwa mabao matano, kosa la kwanza ilikuwa Kwenye mchezo dhidi ya Ihefu, Uwanja wa Sokoine wakati Simba ikishinda mabao 2-1 katika harakati za kuokoa mpira alianua majaro, ngoma ilikutana na mchezaji wa Ihefu akamtungua Aishi Manula alikuwa ni Omary Mponda.
Kosa la pili ilikuwa wakati Simba ikifungwa bao 1-0 na Tanzania Prisons, Uwanja wa Nelson Mandela, alimpoteza Aishi Manula kwenye harakati za kuokoa hatari mpira wa juu uliokutana na kichwa cha Salum Mbangula.
Kosa la tatu ilikuwa Uwanja wa Mkapa wakati Simba ikilazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Yanga kwa kumchezea faulo Tuisila Kisinda iliyoleta penalti iliyofungwa na Michael Sarpong naye alifunga pia bao lake la kwanza kwenye dabi hiyo.
Kwa sasa Simba ina kibarua cha kuiwakilisha nchi kimataifa ambapo leo inatarajiwa kuanza safari kuelekea Nigeria ambapo kitapitia Ethiopia kabla ya kuunganisha mazima mpaka Abuja Nigeria siku ya Jumatano.
Kazi kubwa kwa Sven itakuwa ni kwenye safu ya ulinzi ambayo imekuwa ikiruhusu mabao kwa kuwa inakutana na timu yenye safu kali ya ushambuliaji jambo linalohitaji umakini zaidi.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.
Povel
Natumain sven hata lifanyia kaZi yeye na beki nguli Deni ochien ONyango makosa Kama hayo hayatawez kujirudiah tena kila la kheri Simba. Wa kimataifa peperusheni benderi vzr watanzania tupo nyuma yenu huko
Issa
Hawana. Jipya mikia a bahat yao tu sare wanashangilia
Hopemwaikuka
Mapya haya
aisha
Duuh majanga
Rehema
Majanga tuu
Shakila mrope
Du atari
magdalena
wampe tu muda wamuangalie kama yatajirudia ama lah
Ester jackson
Ni kawaida katika mchezo kama timu ikipata matokeo mabaya basi lazima wa mtupie lawama mchezaji kwani alikuwa yuko pekeake uwanjani kupata matokeo uwanjani lazima mkubaliane nayo na kujifuza na kujirekebisha sio kukatishana tamaa katika klabu
Fatina mfingi
Mmmh makubwa
Sauda
Hatari
Dorophina
Kutupiwa lawama kwa mchezaji ni changamoto kwa klabu ikifanya vibaya tu
Mwajumah
Duuh majanga haya
Angelina
Hizo ni changamoto za mpira
Caroline
Inabidi mjitaidi Aya makosa yasujirudie tena
Rahma
Hatari
Sania
Ni kipindi kigumu sana kwa Onyango
Saupha mohamed
Dhuuu majanga
Tatu
Hizo ni changamoto zinazopatikana ktk mpira
Sarah
Duu majanga
warda
Tutafanyaje sasa tumempenda wenywe