Man City Wapo Tayari Kuachana na Jesus Kumpata Kane

Meneja wa Manchester City Pep Guardiola ameripotiwa kuwa hana shida kuachana na Gabriel Jesus ili kuongeza nafasi ya timu yake kumchukua Harry Kane.

Kane anasemekana kuwa ameiambia Tottenham Hotspur juu ya nia yake ya kuondoka klabuni hapo msimu huu wa kiangazi kusaka mafanikio makubwa.

City wanaaminika kuweka mezani ofa ya kwanza ya pauni milioni 100 kwa nahodha huyo wa England lakini inasemekana wako tayari kuachana na dili hilo ikiwa mwenyekiti wa Spurs Daniel Levy atasimamia msimamo wake wa pauni milioni 150.

Gabriel Jesus
Man City wapo tayari kumuacha Gabriel Jesus aondoke ili waweze kufadhili uhamisho wa Harry Kane toka Spurs

Biashara ya kubadilishana wachezaji sio kipaumbele cha Levy, huku Man City wakiachwa njia panda kufanya maamuzi ambayo yanaweza kuwa kumuuza Jesus mahali pengine kupata fedha za kumnunua Kane.

Kwa mujibu wa Gazzetta dello Sport, Jesus anaweza kuuzwa Juventus wana Serie A wakijiandaa na uwezekano wa Cristiano Ronaldo kuondoka, na Guardiola hataweza kumzuia Mbrazil huyo.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 amefunga mabao 82 na asisti 34 katika mechi 195 za City, lakini mara nyingi aliachwa kwenye benchi wakati Guardiola alipendelea bao tisa za uwongo wakati Wananchi wakikimbia kwa fainali ya Ligi ya Mabingwa ya 2020-21.


KUSANYA PESA HAPA!

IcyGems kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet. Ndio, ukiwa kwenye nyumba ya mabingwa, ndipo utakapoufurahia ubora wa Kasino ya Mtandaoni sambamba na kushinda kwa ushindi mkubwa! Ishi na hii, IcyGems!Meridianbet

INGIA MCHEZONI

Acha ujumbe