Mabosi wa klabu ya Manchester United wameendelea na vikao kwa siku ya pili mfululizo wakijadili hatma ya kocha wa klabu hiyo raia wa kimataifa wa Uholanzi Erik Ten Hag ambaye amekua hana muuendelezo mzuri.
Mabosi wa Manchester United wakiongozwa na Sir Jim Ratcliffe, Dave Braislford, Joel Glazer, Dan Ashworth pamoja na waandamimizi wengine kama kocha wa zamani wa klabu hiyo Sir Alex Ferguson wameonekana nje ya uwanja wa Old Trafford wakielekea kwenye kikao ambacho kinaelezwa mada kuu ni kujadili hatma ya kocha Ten Hag.Mpango unaelezwa ni kuachana na kocha huyo ambaye aliongezewa mkataba mpya dirisha kubwa lililopita ambapo mkataba ungemuweka mpaka mwaka 2026 mwezi Juni, Lakini kutokana na mwanzo mbovu ambao klabu hiyo imeanza nao msimu huu kwenye michuano ya ligi kuu ya Uingereza pamoja na michuano ya Europa.
Kocha huyo ameshindwa kuonesha makali yake ndani ya viunga vya Old Trafford mpaka sasa ndani ya mwaka wake wa tatu wakati ikielezwa amefeli hata kuonesha utambulisho wake wa namna timu inapaswa kucheza kwa maana ya filosofia yake, Hivo wahafadhina wanaona ni kama kocha huyo raia wa kimataifa wa Uholanzi timu imemshinda.
Mabosi wa Manchester United wanaelezwa wameshaanza mazungumzo na makocha mbalimbali kwajili kuchukua kibarua cha kocha Erik Ten Hag, Thomas Tuchel ni moja ya majina ambayo yanatajwa sana kuchukua mikoba ndani ya klabu hiyo lakini kocha ambaye anaelezwa atakaimu nafasi mpaka mwisho wa msimu ni Ruud Van Nestelrooy ambaye kwasasa ni kocha msaidizi klabuni hapo.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.