Klabu ya Manchester United ipo kwenye mazungumzo na kiungo wake kinda mwenye umri wa miaka (19) Kobbie Mainoo raia wa kimataifa wa Uingereza ambaye anafanya vizuri ndani ya klabu hiyo kwasasa.
Manchester United kipaumbele chake kwasasa ni kumuongezea mkataba mpya kiungo Mainoo ambaye tangu amepandishwa timu ya wakubwa amekua na msimu bora sana kumfanya mpaka kuitwa timu ya taifa ya Uingereza kwenye michuano ya Euro 2024 na kufanya vizuri pia kwenye michuano hiyo.Mpaka sasa hakuna makubaliano baina ya pande zote mbili kwa upande wa klabu na mchezaji lakini upande wa klabu unapambana kwa kiwango kikubwa kuhakikisha kabla msimu haujamalizika wanampa mkataba mpya ambao utakua na maslahi makubwa zaidi ya mkataba ambao anao kwasasa.
Kiungo huyo ambaye amekua na ubora mkubwa sana kwenye klabu hiyo na kua moja ya mhimili kwenye safu ya kiungo ya klabu hiyo licha ya umri wake kua mdogo, Hii imekua sababu kubwa ya klabu ya Manchester United kutaka kumuongezea mkataba kiungo huyo ambaye anatajwa kua na kipaji kikubwa.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.