Marcos Rojo Avunjiwa Mkataba Boca Juniors

Marcos Rojo, beki wa kimataifa wa Argentina, sasa ni mchezaji huru baada ya klabu ya Boca Juniors kuvunja mkataba wake, hatua iliyofuata mara baada ya timu hiyo kutolewa kwenye Kombe la Dunia la Vilabu.

Marcos Rojo Avunjiwa Mkataba Boca Juniors

Marcos Rojo alijiunga na Boca mwaka 2021 akitokea Manchester United kwa ada isiyojulikana, akiwa na matarajio ya kuwa miongoni mwa wachezaji tegemeo wa klabu hiyo ya Buenos Aires pamoja na nyota mwenzake wa zamani wa timu ya taifa, Carlos Tevez.

Hata hivyo, miezi michache baada ya kuwasili, Marcos Rojo alijikuta kwenye matatizo baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu katika ushindi wa 1-0 dhidi ya wapinzani wa jadi, River Plate. Tukio hilo lilimfanya apokonywe unahodha kwa mwezi mmoja kufuatia maamuzi ya kocha Hugo Ibarra, ambaye alikuwa na kanuni kali kuhusu nidhamu ya wachezaji wanaofukuzwa uwanjani.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Marcos Rojo Avunjiwa Mkataba Boca Juniors

Licha ya changamoto hizo za awali, Rojo aliendelea kuwa sehemu ya kikosi cha Boca kwa miaka minne, akiichezea klabu hiyo kwenye uwanja wao maarufu wa La Bombonera. Hata hivyo, siku ya Alhamisi, kituo cha ESPN kiliripoti kuwa mkataba wa beki huyo umevunjwa miezi sita kabla ya kufikia mwisho wake rasmi.

Kwa sasa, Rojo anasaka changamoto mpya katika taaluma yake ya soka, huku akiwa huru kujiunga na klabu yoyote atakayoichagua.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.