Klabu ya Arsenal imethibitisha kumsajili kiungo wa Real Madrid na Timu ya Taifa ya Norway, Martin Odegaard kwa mkataba wa mkopo.
Odegaard anaingia Arsenal kuongeza nguvu kwenye safu ya kiungo cha timu hiyo ambapo atawatumikia The Gunners mpaka mwishoni mwa msimu huu.
Taarifa rasmi kutoka Arsenal imetolewa na Mkurugenzi wa Ufundi, Edu ambaye amesema “tunafurahi kumkaribisha Martin mpaka mwishoni mwa msimu. Tunawashukuru Real Madrid na wawakilishi wa Martin kwa kuwezesha usajili huu wa mkopo kufanikiwa.
“Martin ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa na tunaboresha kikosi chetu kwa kuongeza kiungo mshambuliaji kwa muda uliobaki kuelekea mwishoni mwa msimu huu”
Martin Odegaard atavaa jezi namba 11 na huenda akaanza na mechi ya Jumamosi hii dhidi ya Manchester United.
Anayejaribu hawezi kutoka kapa Meridianbet! Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet inakuhakikishia ushindi mkubwa kila unapojaribu kuingia mchezoni. Washindi hushindana, ingia mchezoni!
Sania
Arsenal wameamua kujipanga
Hopemwaikuka
All ze best to him
Rahmal
Habari njema
Magdalena
Habari njema kwa arsenal
Adelta
Arsenal wanajitahidi kwa sasa
Caroline
Karibu Sana
Issa
Saf arsenal
Lydia Emmanuel Magoti
Habari nzuri
Dorophina
Martin kijana Safi sana akiwa uwanjani
Samira
Ni mchezaji mzuri na kwa Arsenal hali iliyonayo kwa sasa atawasaidia
Shakila mrope
Arsenal wanajitaidi kwa kweri
Venerose
Asante kwa makala
Ernest Kimeru
Deal zuri kwa Arsenal