Mashabiki wa Manchester United wameamua kuzuia uwanja wa mazoezi wa klabu huko Carrington wakigoma dhidi ya Wamiliki wa Klabu.
Familia ya Glazers haijafanikiwa katika suala la kuwa na uhusiano mzuri na mashabiki tangia walipoichukua timu hiyo, na uamuzi wa klabu juu ya Super League umefanya mashabiki kuja juu dhidi ya wamiliki.
Mashabiki zaidi ya 15 wa United wameingia uwanjani na kuzuia sehemu za kuingilia wakishinikiza wamiliki kuwajibika kwa kuondoa asilimia zao za umiliki. Mashabiki hao walikuwa wameshika mabango yenye jumbe za kiingereza za ‘51%’, ‘Glazers out’ na ‘we decide when you play’.
Jumbe zote zinashinikiza kuwa mashabiki ndiyo wenye maamuzi na timu, na kuwataka Glazers wajiondoe kwenye umiliki.
Kwa bahati mbaya zaidi, wamiliki wa vilabu ndiyo waliokuwa na neno kwenye sakata la Super League, na kulikuwa na ushirikishwaji mdogo sana wa wahusika wengine kama mameneja na wachezaji. Ujumbe wao unaweza kuwa umefikia mamlaka za United, lakini haifahamiki athari yake katika kubadilisha hali ya hewa ya sakata hili.
Nafasi nyingine kwaajili yako, kasino mpya yenye hadhi ya kipekee inayokupa kila sababu ya kuwa mshindi katika kasino za Meridianbet, anza siku yako na njia rahisi ya kutengeneza mkwanja.
Elika
Dah sio poa kabisa
Johnmary jo
Wakae chini waelewane ili kazi ziendelee #meridianbett#
Adelta
Sio poa
Venerose
Majanga tu
Sauda
Mashabiki noma
Theonestina
Duuuh atar
Issa
Saf
aisha
Duuh noma sana
dorophina
Migomo itaisha kweli bila kutafuta ufumbuzi
Khadija
Hatari sana
Magdalena
Safi sana
[email protected]
Du Nina sana
warda
Mashabiki wanaheshimika sana