Dondoo za masuala ya usajili zimekuwa zikimuhusisha Neymar na kusepa PSG akionekana ameshachoshwa na mshike mshike wa Ligue 1. Neymar alikuwa anahusishwa sana na klabu ya Real Madrid na klabu yake ya zamani ya Barcelona. Taarifa zinadai kuwa Neymar amepewa masharti kadhaa ikiwa anataka kurejea Barca.
Taarifa zinadai kuwa staa huyu alichagua kurejea Barcelona kuliko kwenda Real Madrid. Neymar akiwa PSG, katika msimu uliopita alikukutana na kipindi kigumu sana, pengine ni kigumu zaidi katika soka lake la kulipwa baada ya kupata mikiki mikiki ya majeraha na kujikuta akitumia mda mrefu nje ya uwanja.
Klabu ya Barca, waliripotiwa kuwa wapo tayari kumpokea kijana wao ambaye pia amekiri kuwa kuondoka klabuni hapo ilikuwa ni kosa. Lakini ili aweze kurejea kuivaa jezi ya Barcelona, moja ya masharti ambayo ni lazima akubaliane nayo ni kupungua kwa mshahara.
Soko la uhamisho wa wachezaji linatarajiwa kupigwa vibaya na janga lililoikumba ulimwengu ambalo kwa nafasi yake limeleta athari kubwa katika ulimwengu wa soka na uchumi wa vilabu.
PSG wanajiandaa kumbakiza Neymar na mwenzake Kylian Mbappe na wapo tayari kujitahidi kuwapa kile watakachohitaji. Ikiwa mastaa hawa wataondoka kwa namna yeyote PSG, lazima watakuwa wamepata ofa nzuri zaidi, je ni klabu gani kwa hali ya sasa ipo tayari kuwalipa mishahara mikubwa wanayolipwa PSG ukiacha ada zao za uhamisho?
Kiuhalisia klabu ya Barcelona haifanani na klabu ya PSG kiuchumi, PSG wakitajwa kuwa na pesa zaidi, hivyo Barcelona hawataweza kumlipa Neymar malipo yale yale aliyokuwa akilipwa na PSG. Hivyo kupunguzwa mshahara ni kipaumbele ili staa huyu aivae jezi ya La Liga tena! Ungekuwa yeye?
Barcelona wanamuhitaji nyota huyu pia kukubali kutolipwa baadhi ya bonasi. Wadau wanaamini huenda staa huyu akarejea relini kama akirejea Barcelona kwa sababu ya uwepo wa Messi Barcelona, wawili hawa wanaiva sana wakiwa pamoja.
Theckla
Kila mtu anaangalia maslai yake ye km anaona hamlipi ana sababu yakukataa
Povel
Harud nyumban tumemic sana vitu vyake Asante meridian kwa habar ya kimichezo
Ibrahim
Psg ndo pakukomaa akaze tu
Adelta
Kila mtu anaangalia maslai yake
Isaya massawe
Muda wake unaisha sasa
hamidu
safi. fundi wa mpira brazil & psg# meridianbettz
Tatu
Bora abaki psg kama Barça wanazingua
Neema juma
Apambane tu PSG
Elika
Abakie tu p,s,g ndo panamfaa
Mwajuma
Bora asikilize moyo wake kama unataka arudi Barcelona basi arudi tu
Geniaskaluzwe8
Psg aneangalia masilai
isha
arudi tuu nyumbani tumemmic sana
Lombo
abaki psg
Rehema
Huyo bishooo abaki PSG tu
Hidaya Mohammed
Ridhki popote abaki tu PSG
Antony Luseno
PSG nayo ni timu kubwa atulie tu #meridianbettz
winfrida
arudi tu barca
Salma
Arudi Barcelona
Amani
Bora aende epl kuliko kwenda laliga epl Kuna timu kibao zinamuitaji pia atokutana na hayo makato yote na atakuwa mchezaji wakuangaliwa muda wote
Agness
Muamuzi ni yeye Kama masilai yanalipa arudi barca
Amani
Bora aende epl kuliko kwenda laliga epl Kuna timu kibao zinamuitaji pia atokutana na hayo makato yote na atakuwa mchezaji wakuangaliwa muda wote#meridianbettz
Furahav
Aende tu.
Ester jackson
Inavyoonekana Barcelona hawamuhitaji kama wangemuhitaji wangekubaliana mshahara kwa sababu ya kiuchumi lakini kuweka mashariti sio sahii
mwakalosi
Huyu mpenda pesa hawezi kukubali kupunguza mshahara wake
mwakalosi
Huyu mpenda pesa hawezi kukubali kupunguza mshahara wake huyu bishoo
Swai
Arudi tu nyumbani maana tumemiss Sana 3 twin warudi Kama zamani
Shafii
Kwa kiwango chake kwa Sasa ni Bora tu angekubali kupunguziwa mshahara Barca akifanya vizuri na Barca Bado wakiwa wanamuhitaji ataongezewa tu.
Gabriel
Arud Barca nafas yake bado ipo
Evaluziga
Arudi tu nyumbani tume miss sana
Zeiyana iddi
Neymar bishoo sana..!ubishoo ukizidi sana utaaribu kipaji chako acha ustaa
Lydia Emmanuel Magoti
Arudi tuu Barca
Ernest
Hapa Neymar anawakati mgumu sana, anakazi ya kuchagua swala la mapenzi na klabu na Mkwanja!!!!
Fatina
Arudi nyumban
felister
kuangalia maslai ni vizuri lakini Mimi namshauri abaki tu psg
David pere
Kwake limekuwa Shakti kubwa Ndio maana limemshinda
SADICK
Nimekuwa nikishuhudia maamuzi mengi mabaya ya wachezaji wa Brazil wakati wa usajiri. kama Neymar hajapata alilotaka akiwa PSG sioni maajabu atakayopeleka Barcelona.
Ester mmakasa
Masharti yao magumu ,ila kama mwenyewe karidhia basi sio mbaya.
Frank patrick
Kwaajili ya ulinzi wa kipaji chake akubali tu hayo masharti
Samira
Messi anakubalika sana barcelona na kipaji chake kitakua sana kuliko psg
Dorophina
Ni bora arudi barca
Samiah
Messi anakubalika sana Barca
Asia Abdy
Hana jipya abaki PSG
Asha
Harud nyumban tu Asante meridian
Nasra
Rudi nyumbani messi
Mwanaidi
Arudi alipotoka bhna
Magdalena
Bora arudia maana tumemic mambo yake
#meridianbet