Mbappe Ashinda Katika Mzozo wa Haki za Picha

Mchezaji wa klabu ya Psg Kylian Mbappe ameshinda katika mzozo wa haki ya taswira yake naΒ  Shirikisho la Soka la Ufaransa (FFF) baada ya Shirikisho hilo kuthibitisha kwamba “itarekebisha” makubaliano yake na wachezaji wa Ufaransa.

 

Mbappe Ashinda Katika Mzozo wa Haki za Picha

Mshambuliaji huyo wa Psg alihusika kutoelewana na FFF tangu Machi, alipokataa kujitokeza kupiga picha iliyoandaliwa kwaajili ya timu ya vijana wa Ufaransa . Mbappe alikuwa na hamu ya kupata udhibiti mkubwa wa taswira yake ili kuepuka kuhusishwa na chapa fulani, Lakini Rais wa FFF Noel Le Graet na msafara wa mchezaji huyo hawakuweza kufikia maelewano walipokutana mwezi Juni.

Le Graet iliiambia L’Equipe hawakuwa na muda wa kutosha wa kufanya mabadiliko yaliyoombwa kabla ya Kombe la Dunia kwa hivyo, timu ya Mbappe ilithibitisha Jumatatu kuwa atasusia tena upigaji picha uliopangwa kupigwa Jumanne baada ya timu kujipanga tena kwa mechi zijazo za ligi ya Mataifa dhidi ya Austria na Denmark.

 

Mbappe Ashinda Katika Mzozo wa Haki za Picha

Lakini baada ya mkutano uliofuata uliohusisha maafisa wa FFF siku ya Jumatatu, hatimaye aliamuliwa kukubaliana na matakwa ya Mbappe.

“Baada ya majadiliano ya mwisho mbele ya watendaji wa timu ya Ufaransa , Rais, Kocha na Meneja wa Masoko, Shirikisho la Soka la Ufaransa linajitolea kurekebisha, haraka iwezekanavyo, makubaliano yaliyomo katika haki ya picha inayoiunganisha kwa wachezajiΒ  wake katika uteuzi.

FFF inafuraha kufanyia kazi muhtasri wa makubaliano mapya, amabayo hayatairuhusu kuhakikisha maslahi yake huku ikizingatia maswala halali na hukumu iliyoonyeshwa kwa pamoja na wachezaji wake.

 

Mbappe Ashinda Katika Mzozo wa Haki za Picha

Acha ujumbe