Mshindi wa kiatu cha Dhahabu cha Ligue 1, Kylian Mbappe anaamini wanatakiwa kugawana tuzo hiyo na Wissam Ben Yedder baada kufungana kwa magoli 18 wote.
Mbappe alitangazwa kuwa mfungaji bora wa Alhamisi baada ya msimu kumalizika kwasababu ya Corona.
Straika PSG amemaliza akiwa na magoli sawa na mshambuliaji wa Monaco, Ben Yedder, lakini ametwa tuzo hiyo kwasababu alifunga magoli mengi kwa jitihada binafsi.
Magoli matatu ya Ben Yedder yalikuwa penati lakini Mbappe anaamini mchezaji mwenzake wa Ufaransa, anastahili kutambuliwa.

“Asante kwa meseji zenu. Nafikiri Wissam pia anastahili tuzo kama Premier League walivyofanya msimu uliopita katika utoaji wa tuzo,” Mbappe amesema kwenye kurasa wake wa Twitter akamalizia kwa kusema ‘Taji kwa Wissam’.
Ben Yedder akasema: “Asante kaka, hongera kwako… Tutafanya namna kama utataka.”
Kumbukumbu ya Mbappe kwe Premier League inahusu tuzo ya kiatu cha Dhahabu 2018-19 ambacho kiligawanywa sawa kwa nyota wa Arsenal, Pierre-Emerick Aubameyang na Liverpool, Sadio Mane na Mohamed Salah, wote walikuwa na magoli 22.
Kwa Mbappe, hii ni mara ya pili mfululizo nyota huyo kutwaa mfungaji bora wa Ligue 1. Ligi ilimalizika rasmi wiki iliyopita, na PSG kutangazwa mabingwa, wakati Toulouse na Amiens wameshuka daraja.



Ester mmakasa
Hakuna kama mbappe.
Emmy cleopa
Mbappe yupo vzr namkubali sana
Frank Patrick
Maamuzi ya kimpira busara kabisa
SADICK
Mbappe ni muungwana sana, baada ya Ufaransa kubeba kombe la Dunia fedha zote alizopata alitoa msaada.
felister
mbappe nlianza kumuelewa wkt anacheza kombe la dunia kwny timu yk ya taifa
Adelta
Mbappe Ni muungwana
Na anajuwa mpira
Gabriel
Habar nzur
Lydia Emmanuel Magoti
Akuna Kama mbape anajua
Ester jackson
Mbappe ana roho ya kipekee anapenda haki sawa
Asia Abdy
Mbape mchezaji mwenye umri mdogo lkn anafanya vyema
Rehema Dickson
Mbappe anajua sana na anastahili kilicho bora 💯
Neema hassan
Mbappe jembee..
Shafii
Mbape akaze ivo ivo atakuja kuweka record zake nzuri duniani
Ernest Kimeru
He is a world class player and professional, That is a classy act of sportsmanship.
Aziza
Mbappe yupo vizuri sanaa💯
Mwajuma
Namuelewa sana mbappe jembe laPSG
Rehema
Hiyo habari iko fresh
Furahav
Anajua kulichungulia gol.
Hamidu
Talent player
Lombo
mbappe yuko saf sana
Geniaskaluzwe8
Habari jema sana
Pove
Asante meridian kwa habar ya kimichezo
Neema juma
Mbappe namkubalii kichiziii
Tahiya
Yuko vzr
winfrida
mbappe mtu mbaya
Jenifer
Ana moyo wa peke ake 😅😅😅mm nisingeweza kwa kweli uongo dhambi
Nasra
Yuko Poa
Salma
Anajuwa akaze buti atafika mbali
Njiku
Mbappe yupo poa sanaa
Zainabu
Vizuri lakini watagawanaje hiyo tuzo mbappe anastahili
Dorophina
Mbape ni noma
Theckla
Mbappe ana hekima sana
aisha
namkubali mbappe yuko vizuri
Fatina
Yuko vinzur sanaa
Isaya massawe
Mbape yuko vizur sana
Evaluziga
Mbappe Yuko juu
Adelta
Mbappe Ni muungwana
Na anajuwa mpira
David pere
Huyu dogo noma Sana
Issa
Ni vizur kwake