Nyota raia wa Argentina na klabu ya Barcelona, Lionel Messi ameshinda tuzo nyingine ya Ballon d’Or baada ya kuwashinda wapinzani wake aliokuwa akichuana nao. Ikumbukwe kwamba kulikuwa na kundi kubwa la washindani lakini watatu wa nafasi za juu ambao ni Virgil Van Dijk na Ronaldo walifanikiwa kusogea karibu zaidi.
Soka ni mchezo ambao haufichiki ikiwa na maana kwamba upo wazi sana kwenye historia yake. Ronaldo hajawa na msimu mzuri sana hata alipohamia Juventus msimu uliopita labda kikosi chake kikipata utulivu huenda akawa na uwezo wa kung’ara zaidi. Hata umri wake umesogea zaidi kwa kipindi hiki.
Usiku wa kuamkia leo ulikuwa na historia mpya kwa Messi ambaye hadi sasa anaongoza kwa kunyakua tuzo hiyo akiwa na jumla ya tuzo sita za namna hiyo! Uwezo wake aliounesha ikijumuishwa na mchango wake ndani ya Barcelona msimu huu vimeweza kumpa alama nyingi zaidi mbele ya wapinzani wake.
Nyota wengi wameunga mkono kampeni za mwaka huu hadi Messi kunyanyua tuzo hiyo lakini wakishutumu kwamba Ronaldo aliporwa tuzo yake mwaka 2018 katika kipindi ambacho alikuwa na haki ya kunyanyua tuzo hiyo. Ni kipindi ambacho wengi hawakukubaliana sana na matokeo yaliyotolewa kwamba haikuwa halali kumpora tuzo ile kwa mafanikio aliyoyaonesha.
Kwa miaka kumi tuzo hiyo imefanikiwa kutoka katika mikono ya wawili hao yaani Messi na Ronaldo mara moja ambayo ilichukuliwa na Modric japo ilikuwa na utata pia. Kwa kipindi kirefu utawala wa mastaa wawili hao umekuwa ni wa kubadilishana tu akichukua mmoja mwaka unaofuata anainyanyua mwingine.
Chiellin ambaye anacheza na Ronaldo pale Juventus ameweza kukubaliana na ushindi huo wa Messi kwa msimu huu kwa kusema kwamba ni sahihi kabisa kwa nyota huyo kunyanyua tuzo hiyo msimu huu lakini hakuridhishwa na maamuzi yaliyotolewa msimu uliopita kwamba nyota wao huyo alipokwa tuzo yake.
Anaamini kwamba picha zima lilichezwa na Madrid ambao hawakutaka nyota huyo ashinde tuzo kwa sababu alikuwa nje ya kikosi chao lakini anaamini ndani ya kikosi chao ni wakati fulani tu wanapitia ila wakati unakuja wataweza kurejea kwenye ushindani na kuwafanikisha kukaa kwenye ramani nzuri ya kisoka zaidi.
Mbali na Messi wengine walioshinda tuzo ni Rapinoe upande wa wanawake na Allisson tuzo ya Yachine.
Ester jackson
Uwezo wake aliounesha ikijumuishwa na mchango wake ndani ya Barcelona msimu huu vimeweza kumpa alama nyingi zaidi mbele ya wapinzani wake.