Tuchangamshe akili kidogo na maswali kuntu katika udadavuzi wa suala la Messi na Barcelona hasa baada ya taarifa iliyoibua gumzo kwenye vichwa vya habari za michezo.
Unaweza kufikiria kama Messi Anawalipa Barcelona au Barcelona Wanamlipa Yeye?
Unaweza kushangaa hii inakuwaje, lakini licha ya ukweli kuwa Barcelona wanaonekana kutokuthamini sana mchango wa Leo klabuni hapo kutokana na namna walivyolifanyia kazi suala la mkataba wake alipoamua kuondoka klabuni hapo, staa huyu ameonekana kuwa sehemu muhimu zaidi kwenye mapato ya klabu hiyo.
Kwa mujibu wa Diario Sport, taarifa zilizovuja juu ya mkataba wa Leo na klabu ya Barcelona zimebainisha kuwa nyota huyu anachangia kwa takribani asilimia 30 ya mapato ya klabu.
Taarifa za mkataba huo zinasema kuwa kwa makataba aliosaini Leo tangia mwaka 2017, ameigharibu Barcelona €383m tangia aliposaini mkataba huo, lakini amechangia pato la jumla ya €619m nyongeza ya zaidi ya €235.
Hivyo ukiacha ukweli kuwa Messi amekuwa akiwapatia magoli kibao Barcelona na kuwavusha viunzi vingi vya ligi na michuano mingine, nyota huyu ni sehemu muhimu katika pato la klabu, klabu inapaswa kujivunia staa huyo kama uwekezaji zaidi ya kuona ni kiasi gani wanamlipa.
Neptune’s Richies ni mchezo Unaokupa pesa chap chap huku ukiwa unaburudika kupitia Kasino ya Mtandaoni ndani ya Meridianbet.
Caroline
Uyu Messi uyu ataondoka tu Barcelona
Magdalena
Wao wenyewe wakae na uongozi waelewane
Hopemwaikuka
Wanategemeana buana
Dorophina
Hapo brca wanawajibu wa kumlipa mnyama kwa kazi aliyoifanya kuisaidia timu
Lydia Emmanuel Magoti
Hapo ni kuerewana tuuu akuna jinsi
Sania
Hapo kuna kazi kubwa
Sarah
Cha muhimu nimaelewano tu
Issa
Mess noma
samiah
Noma Messi
Janeflora malisa
Hatar kwa messi
Venerose
Asanteni kwa taarifa
warda
Labda wanalipana