Klabu ya AC Milan imeripotiwa kuanza mazungumzo na nyota wake Frank Kessie kwa ajili ya makubaliano ya mkataba mpya.
Nyota huyu ambaye ni raia wa Ivory Coast ameweza kuwa sehemu muhimu ya Kikosi cha Pioli pale San Siro wakati mkataba wake wa sasa ukifika tamati Juni 2022.
Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari za michezo, Milan sasa wanafanya kazi mazungumzo ya wachezaji wao watatu ambao mikataba yao inakaribia kuisha.
Wachezaji ambao wanatajwa kuwa mazungumzo juu ya hatma ya mikataba yao mipya yanaendelea ni pamoja na Zlatan Ibrahimovic, Gianluigi Donnarumman na Hakan Calhanoglu.

Hata hivyo, kwa mujibu wa La Gazzeta dello Sport, klabu hii imeanza mazungumzo na Kessie pia.
Kessie ameshiriki katika mechi 9 Milan msimu huu wa Serie A. Amefanikiwa kupata magoli matatu na asisti 2 mpaka sasa.
Nyota huyu anaweza kufikisha idadi ya mechi zake 150 kwa klabu hiyo dhidi ya Celtic Alhamisi hii. Anaikamilisha idadi hii kwa mda wote aliyokuwepo klabuni hapo tangia alipotua kutoka Atalanta mwaka 2017.
Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!




Angelina
Niceupdate
Johnmary jo
Kila raheri #meridianbett#
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri sana
lombo
habar njema
Magdalena
Milan watakuwa wamepata jembe
Sabrina
Itakua poa sana kama Frank akiendelea kusalia milan
Fatina mfingi
Millan wamepata mchezaj mzur
Caroline
Kessie amekua na msimu mzuri
Dorophina
Frank yupo vizuri milan wasisite kwa hilo
Tatu
Habari njema
Povel
Kila la kheri milan
Issa
Safi
Hopemwaikuka
Vzur
Janeflora malisa
Safi
Mariam mtandama
Safi
warda
Wampe tu mkataba Frank