Al-Rayyan wamepata pigo kuelekea maandalizi ya msimu mpya, baada ya mshambuliaji wao wa Kiserbia Aleksandar Mitrovic kupata majeraha. Taarifa rasmi ya klabu imesema, “Mchezaji wetu Aleksandar Mitrovic amepata jeraha kwenye ligament ya mguu wa kushoto, baada ya kugongana kwa nguvu wakati wa mazoezi ya timu.”

Vipimo vya kitabibu vimeonyesha kwamba Mitrovic atalazimika kukaa nje kwa muda wa kati ya miezi miwili hadi mitatu. Kwa sasa yupo kwenye mpango kamili wa matibabu na ukarabati chini ya usimamizi wa benchi la ufundi na madaktari wa klabu, ili kuhakikisha anarudi kwa nguvu haraka iwezekanavyo.
Mitrovic, mwenye umri wa miaka 31, alijiunga na Al-Rayyan Septemba 2025 akitokea Al-Hilal. Tangu kuwasili, ameshacheza mechi 14 na kufunga mabao 7 pamoja na kutoa asisti 4. Kabla ya hapo, alitamba sana akifunga mabao 68 katika mechi 79 akiwa Al-Hilal, na pia akiacha rekodi kubwa England na Fulham kwa mabao 111 katika mechi 206.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kocha mpya Luka Catani ameipeleka Al-Rayyan nchini Hispania kwa kambi ya maandalizi, ambapo walitoka sare ya 3-3 dhidi ya Rochdale ya England kwenye mechi ya kirafiki. Hata hivyo, kukosekana kwa Mitrovic kunabaki kuwa changamoto kubwa kwa kikosi kinachotegemea sana mabao yake.

Kwa mashabiki wa Al-Rayyan, jeraha hili ni pigo, lakini pia ni mtihani wa kuona jinsi kikosi kitakavyoweza kusimama bila nyota wao. Mtihani unabaki kuwa kama washambuliaji wengine wataweza kuziba pengo lake hadi atakaporejea.


