July 16 1986 kule cardif Wales alizaliwa Gareth Bale (mkombozi) akiwa mchanga sana baba yake mzee Debbie Bale alimpeleka katika shuke moja ya kanisa la Whitchurch ili apate elimu ya dini na maarifa ya soka.
Alipopata mafunzo ya kutosha, bale akachagua kucheza nafasi ya beki wa kushoto katika maisha yake. Ikawa hivyo mpaka alipojiunga na Southampton mwaka 2006, na 2007 Bale akajiunga na Tottenham Hotspur kama beki mchanga kabisa EPL na kucheza miaka 6 kama beki.

Mwaka 2012 kocha wake Andre Villas Boas akamuita pembeni na kumshawishi ahame namba na kucheza kama winga kutokana na uwezo wake mkubwa. Tangu hapo bale akawa wamoto kweli kweli. Uwezo wa bale umenirudisha mpka Bunju pale Mo simba Arena kuitazama miguu ya Mohammed Hussein.
Mwalimu Amunike alimtumia kama winga pale Taifa stars lakini Sven vanderbroek anamtumia kama beki, Binafsi napenda kumuita GENERATOR, ameutawala upande wa kushoto kwenye ramani ya Tanzania, nanyoosha kidole cha shahada kushuhudia ufalme wa Zimbwe kwenye kiti cha enzi juu ya nyasi za Tanzania. Itoshe kusema inatosha Zimbwe kucheza Tanzania.

🎶Pasi zake temethali, zinatibu na kuenzi, krosi zake manuwari akipiga hakopezi. 🎶.. ooh Zimbwee…Bila shaka huyu ndie mchezaji bora wa raundi ya kwanza kwa Simba msimu huu. Ukiachana na skills zake Zimbwe wa leo sio wa jana. Ameimarika kwenye kukaba na kulinda. Wapo wanaokaribia uwezo wake lakini wanatakiwa kujifunza mengi kupitia yeye.

Yupo Edward Charles Manyama wa Namungo, yupo Yasin Mustafa wa Yanga na Bruce Kangwa wa Azam. Hawa wote ni mafundi wenye haiba ya kufanana na Zimbwe Jr. Wakijinoa zaidi basi Ligi yetu itanawiri sana upande wa kushoto.

Asante kwa burudani Zimbwe. VPL imekufungulia dunia, sasa ni kazi yako wewe kuwa unachotaka. Sitashangaa kukuona ukicheza Ulaya mahala penye hadhi kwako, ila nitaumia nikikuona unastaafu ukiwa Tanzania, na hiyo ndio itakua tafsiri ya dhambi ya usaliti. Chonde chonde usije kutusaliti. Go Zimbwe go.

VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???




Tatu
Makala nzuri
Shakila mrope
Asant kwa taarifa meridian bett
Lydia Emmanuel Magoti
Bonge la makala hipo vizuri
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif meridianbet
Sarah
Makala iko poa sana
Angelina
Goodupdate
Rahmal
Asante kwa makala nzuli
Hopemwaikuka
Mnatujuza meng kwakwel
Issa
Zimbwe saf sana
Ernest Kimeru
Kijana yupo vizuri sana
Dorophina
Zibwe yupo vizuri sana
warda
Hussein yuko poa sana