Jiji la London ni miongoni mwa majiji mashuhuri duniani. Linapatikana katika nchi ya Uingereza. Ukipata fursa ya kutembelea jiji hilo hasa maeneo ya Fulham basi hakikisha unapita sehemu hizi: kama wewe ni mpenzi wa maakuli usiache kupita Ice and Slice Restaurant, hapa utapata vyakula vya asili vya Uingereza. Hautojutia muda wako. Kama wewe ni mpenzi wa vito vya thamani kama pete za dhahabu, hereni au bangili basi Circa Vintage ndo’ chaguo lako sahihi. Na kama wewe ni mpenzi wa soka, bado hujazuru Fulham London vya kutosha kama utaondoka hapo bila kutembelea makao makuu ya timu kubwa Uingereza na duniani kwa ujumla, Chelsea FC.
Chelsea ni timu yenye historia kubwa tangu kuundwa kwake mwaka 1905. Ukongwe wa timu hiyo unafanya kuweko historia kadhaa ambazo zinawekwa na kusahaulika klabuni hapo, lakini kamwe hapatotokea kusahaulika miaka ya dhahabu ya mshambuliaji wao hatari Didier Drogba.
Nyota huyo mwenye asili ya Afrika amejijengea heshima yake ndani ya klabu ya Chelsea na anaendelea kuheshimika na mashabiki hata viongozi mpaka leo. Mashabiki hao hawatomsahau John Terry, hawatomsahau Frank Lampard. Lakini kwa gharama yoyote watazidi kumkumbuka Didier Drogba. Jamaa alikua anajua wajibu wake wa kufunga magoli, yeye akaifanya hiyo kuwa ni sehemu yake ya maisha. Kufunga!
Ukitaka kuona ukomo wa hasira za mashabiki wa Chelsea waambie Drogba hakuwa bora, lakini ukitaka kuona hasira zao zikivuka mipaka we’ jaribu kushindanisha Grogba na mchezaji mwingine wa zama zake. Tena ukitaka uwakere zaidi mpe ushindi huyo mchezaji wako mwingine, hawatokuelewa!
Nyota mwingine wa zamani wa Barcelona Samuele Eto’o ametaka kuziona hasira hizo, Eto’o amenukuliwa na mtandao wa Goal akisema yeye alikua bora kuliko El Hadji Diouf na Didie Drogba. Mashabiki wa Chelsea mnasemaje hapo?
Eto’o alisema hayo akimjibu Diouf ambaye siku kadhaa zilizopita alichapisha video katika mitandao ya kijamii akijigamba kiwa yeye ndio mchezaji bora wa muda wote Afrika. Drogba na wachezaji wengine wakubwa Afrika bado hawajajibu hili lakini Eto’o hajataka kuliacha lipite.
“Hakuna hata mmoja kati yao (Drogba na Diouf) aliyekuwa anafikia uwezo wangu au kunizidi, katika maisha yangu yote ya soka nilitaka kuwa namba moja na kwa hakika ilikuwa hivyo” Eto’o.
Ni kweli kuwa Eto’o alikua namba moja katika maisha yake yote ya soka? Mimi nakupa takwimu jibu utatafuta mwenyewe. Tena kaa nalo usimwambie mtu.
Etoo alichezea vilabu vikubwa Ulaya kama vile Inter Milan, Barcelona na Chelsea. Elishabeba tuzo ya mchezaji bora Afrika mara nne, na akawa mshindi namba tatu katika tuzo ya FIFA ya mchezaji bora wa dunia mwaka 2005 nyuma ya Ronaldinho na Lampard.
Akiwa Barcelona alibeba La Liga mara tatu, Copa Del Rey mara moja, na kombe la ligi ya mabingwa Ulaya mara mbili.
Akiwa na Inter Milan alifanikiwa kuchukua taji la Seria A mara moja, Coppa Italia mara mbili mfululizo, ligi ya mabingwa Ulaya ‘UCL’ mara moja, na taji la FIFA la klabu bingwa ya dunia mara moja.
Mafanikio ya Eto’o hayaishii katika ngazi ya vilabu. Hata ndani ya timu yake ya taifa alishafanikiwa kubeba medali ya dhahabu katika mashindano Ya Olympics yaliyofanyika mwaka 2000, kisha mwaka huo huo akashinda kombe la afcon kabla hajafanya hivyo tena mwaka 2002.
Swali kwa mashabiki wa Chelsea, kwa hizo rekodi za Drogba unazozifahamu je, zinamfanya Drogba kuwa chini au zaidi ya Eto’o? Jiulize kisha majibu kaa nayo.
Zeiyana iddi
Etoo..!hanajua sana
Gabriel
Sio mkal tu jamaa anajua tena n mchezaji ambaye aliyelipwa hela nying kwa bara la Africa aliyechezea ulaya
Tahiya
Etoo ni noma sana
Emmy cleopa
Etoo yupo vizur “meridianbettz
Lombo
drogba juuuuuu
Asia Abdy
Etoo anajua
Povel
Didier goal drogba tembo wa ivory coast. Mfalme darajan London yupo juu thanks meridian kwa update
felister
Eto’o baba lao
Evaluziga
Drogba Yuko juu
mathayo sonje
Mnyama Drogba ni balaaa maana aliyoyafanya sote tumeona paleee darajani
David pere
Wote Kama wanalingana Ila eto’o kamzidi kidogo
Ester jackson
Eto’o
Adelta
Namkubali Sana Eto
Samiah
Eto bonge la kiungo
Salma
Nimchezaj mwenye viwango vyake africa
Amani
Wote Kama wanalingana Ila eto’o kamzidi kidogo drogba kwa sababu eto,o amecheza timu nyinginyingi
Theckla
Drogba anatisha
Mwanaidi
Drogba ndio zaidi
Antony Luseno
Drogoba ni hatari
Mwajuma
Eto yupo vizuri
Hope mwaikuka
Etoo nomaa
Lydia Emmanuel Magoti
Wachezaji hote niwazuri nahote kila mtu hana upiga mpira nakilamtu akikasehemu yake halio pangwa lazima hai tende kaz
Neema hassan
Eto’o fundiii
Theonestina
Drogba mkali
Rehema Dickson
Eto’o baba lao
Ester mmakasa
Wote wanafanya vizuri sana kwenye soka
Carolyne
Drogpa ni habari nyingine
Hidaya Mohammed
Eto’o hana mpinzani
Kenani
Mote wakali
Kenani
Hii nimeipenda
aisha
Etoo mkali
Neema juma
Anajijua na anauwezo mzuri Eto’o wewe ni hatariii
Mwanahamisi
Wote mafundi
Juliana
Mmmmh! ila Eto’o mkali aise
Furahav
Mmh kwan huyo Drogba alikuwa anamiguu minne?
winfrida
drogba namkubali yuko vzr
Ernest
Eto’o Mkali hapa hana mpinzani na ukweli ni kama antena juu wa bati ipo wazii tuu.
Genia Sikaluzwe
Drogba noma sana
Swai
Eto’o yuko vizuri sana ni 🔥🔥🔥
Magdalena
Etoo #meridianbet
Warda
Aisee mmenitajia mgahawa wangu Ice and slice Restaurant daa nishakula na drogba hapa #Meridianbettz
Dorophina
Etoo ni mkali kuliko na anakiwango cha juu
mwakalosi
Kimafanikio etoo hana mpinzani katika Africa
Isaya massawe
Etoo yuko vizuri kuliko
Hamidu
Samwel etoo # meridianbettz
Khadija
etoo tupo vzr
frank patrick
Etoo alikuwa zaidi ila majibu yangu ndugu mwandishi umenambia nikae nayo
Shafii
Wote nawakubali ila etoo jembee sanaaa
Maleek Jigga
Etoo ni alikua zaidi ya wote hao..
Maleek Jigga
Etoo ni alikua zaidi ya wote hao..
farida ahmadi
Wote wakali Sana etoo mkali pia ht drogba mkali kiukweli wamesaidia San timu zao