Imeripotiwa kuwa klabu ya soka ya Newcastle United imeingia katika makubaliano na klabu ya Barcelona kuhusiana na dili lao la winga Philippe Coutinho.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 ambaye kwa sasa yupo kwa mkopo katika moja ya klabu za ligi kuu ya Ujerumani, Bundesliga, Bayern Munich, anaonekana hatoendelea kukaa kwa Barca wakati ambapo jamaa hao wa Premier League wakiwa wanamvizia ili wamsajili kwao.
Ripoti za hivi karibuni zinasema kuwa nao Arsenal walikuwa wakimuwinda kwa udi na uvumba na huenda wanamsaka mpaka sasa hivi, ila pesa ya kumchukua ambayo ni £300m kutoka kwa Newcastle inaweza kuwafanya The Magpies kuvunja vibubu vyao ingawa kuna shida za kiuchumi kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Coronavirus.
Kwa sasa, Mundo Deportivo wanadai kuwa klabu hiyo ya Steve Bruce imewasiliana na klabu ya soka ya La Liga, Barcelona juu ya uwezekano wa kukamilika kwa dili la Coutinho, ambaye atakuwa naye akihusika katika makato ya mishahara yaliyotokana na matatizo ya kiuchumi katika vilabu vingi duniani.
Mchezaji Coutinho amefunga jumla ya mabao nane na kutoa assists sita kwenye Bundesliga msimu huu lakini mchezaji huyo wa zamani wa Liverpool anaonekana wazi kuwa hatoichezea klabu ya Bayern kwa mara nyingine kutokana na majeraha ya kifundo cha mguu.
Klabu hiyo inayoongoza katika msimamo wa Bundesliga walikuwa na chaguo la kumsajili mwanasoka huyo wa kimataifa kutoka taifa la Brazil kwa mkataba wa kudumu lakini waliamua kuachana na dili hilo.
Wasikate tamaa wajaribu kuendelea na jitahada za kumpata na wampe mkataba wa kudumu
philippe uko vizuri sana sio kwa kusakwa uko ila bidii yako ndio inasababisha, endelea kukaza
Ni mchezsj mzur wapambanie tu kumpata
Coutinoh uko vzr sn
wajaribu kuendelea na jitahada za kumpata na wampe mkataba wa kudumu
Wamshawishi kwa donge nono atakubali tyuu
Kizuri kinatafutwa! Endeleeni kumpambania
Philippe Yuko vizuri sana
Ila aongeze bidii
Wasikate tamaa wajaribu kuendelea na jitihada za kupambana na wampe mkataba wa kutubu
Dili nono aise
Mchezaji mahiri uwanjan wapande dau nono watampata…
Huyo courtinho alikosea mno kuondoka Liverpool sasa hivi kiwango kimeshuka
kizuri kinajiuza big up courtinho
Philippe Yuko vizuri sana
Ila aongeze bidii
Wajaribu kuongea na uongozi wake ili waelewane kama watamtoa .
Wasikate tamaa wapambane hadi wafanikiwe
Phillippe namkubali sana
Sasahivi ni usajili tu #Meridianbettz
chaguo la kumsajili mwanasoka huyo wa kimataifa kutoka taifa la Brazil kwa mkataba wa kudumu lakini waliamua kuachana na dili hilo#meridianbettz
Asante kwa taarifa
Coutinho bora akubaliane na dili hilo
Newcastle ni team ya level yake kweli?
Ahsante kwa taarifa
Itakua bonge la deal endapo wakimpata
Mabosi wapya kweli hawataki mchezo wanataka kufanya mapinduzi ya kuchukua makombe
Ahsant sana meridianbet kwa taarifa
bora atue man united atapata no na pesa nzuri
Wangempata ingekua vizur maana ni mchezaji Mzuri
New Castle tuachieni coutinho wetu si size yenu
Countinho yupo vzr sana
Countinho n mchezaji mzur hivyo itabid nae aangalie mslai
Ni mchezaji mzuri wa mbambanie tu kumpata
Wakimchukua tu watakuwa wababe wapya EPL
Itakua good Sana Kama ukimpata
Kama Newcastle itahitaji kurudisha heshima yake kwenye ulimwengu wa soka basi Coutinho sio mchezaji wa kumuacha wakati huu.
Coutinho kawa kama kambale tu hana budi kwenda kuishi matopeni maana maji yamekauka
Coutinho kwenda Newcastle moja ya deal zuri sana..njoja tusubiri kipi kitajili! meridianbettz
Asante meridianbet #kwa taarifa
Hatma imekuwa mbya kwa Coutinho kuondk kwake liverpool kunamgharimu sasa
Coutinoh uko vzr sn
Newcastle wanajipanga na mashambukizi zidi ya wapenzani wao..!naimani ligi msimu wa pili utakua baraa