Rafiki yangu mmoja alinipigia simu kuniuliza maoni yangu juu ya Gareth Bale. Kwanini hataki kuondoka Real Madrid wakati ameshaambiwa kuwa hatakiwi na hayupo kwenye mipango? nilimpa jibu jepesi tu, ‘PESA’. Sijui kama alinielewa. Ila hiyo ndiyo sababu. PESA tu! Hakuna kingine.
Basi wakati namuelezea kwanini pesa ndio inamuweka Gareth Bale Madrid, kichwani mwangu akanijia mtu aliyeitwa Winston Bogarde. Beki wa kiholanzi aliyesajiliwa na Chelsea mwaka 2000. Alisajiliwa akitokea Barcelona akiwa na miaka 29 tu na kocha Gianluca Viali. Alisaini kandarasi itakayompatia mshahara wa paundi arobaini elfu kwa wiki.

Hii pesa ni nyingi sana. Mateo Guendouzi kwa sasa anatamba pale London kwa mshahara kama huo. Fikiria miaka 20 iliyopita ilikuwaje. Ilikuwa nyingi zaidi. Basi Bogarde akasaini mkataba wa miaka minne na Chelsea. Haukupita muda Vialli akafukuzwa, akaletwa Claudio Ranieri.
Ranieri hakumtaka Bogarde, akashauri auzwe. Chelsea ilimtafutia timu, ila hawakufanikiwa kwasababu ya mshahara wake. Hakuwa tayari kupunguza mshahara ili apate timu. Hakuwa tayari kuondoka kwa mkopo. Chelsea wakamshusha afanye mazoezi na timu ya watoto. Bogarde hakujali, yeye alichowaza ni pesa tu aliyokuwa anapatiwa.

Alimaliza mkataba wake na Chelsea mwaka 2004 akiwa amecheza mechi tisa tu. Akaamua kustaafu na kwenda Marekani kula pesa aliyoivuna Chelsea kwa miaka minne. Hata hivo, maisha yanahitaji nini tena zaidi ya pesa? Sidhani kama lipo jibu. Bogarde alijua hili, ndio maana hakuchezea nafasi aliyopata ya kuchuma noti.
Basi mawazo kama haya anaishi nayo binadamu aitwaye Gareth Frank Bale. Analipwa kuliko mchezaji yoyote yule Real Madrid. Sasa hawamtaki na wamemuambia wazi, ila yeye hajali. Anachojali ni kuona paundi 350,000 zikiingia kwenye account kila wiki. Maisha yanataka nini tena?

Kama ni mataji ameshanyanyua ya kutosha. La Liga, Copa del rey, UEFA. Anataka nini tena zaidi ya pesa? Anajua kwa umri na uwezo wake hawezi kupata timu itakayomlipa ‘kibingwa’ kama wanavomlipa Real Madrid kwa sasa. Kumbuka Bruno Fernandes anakula paundi laki moja kwa wiki. Sasa kwanini Gareth Bale aondoke? Tumuache apige pesa.
Beti Mbio za Mbwa Mubashara
Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.


Ernest
Bale amenifurahisha sana nadhani Binafsi ana cha kupoteza ila anataka kuikomoa Madrid na Zidane
magdalena
bale yupo vizuri sana na navyoona sidhani kama ana mpinzani
Mwajumah
Bale hana Cha kupoteza ila anataka kuikomoa Madrid na Zidane tu kwa ninavyoona binafsi#Meridianbettz
Fatina mfingi
Bale yupo vizur
Fatuma kasomo
Jamaa yupo vizuri sana
Nasra
Ajawahi kukosea bale
Njiku
Safari ya bale inafurahisha sana real madrid kwa mimi naona kama atamaliza na nao real madrid arudi nyumbani ili kuongeza chachu ya ushindani so naona arudi tottenham
Caroline
Haaa Bale nimekupenda bure
Adelta
Bale good 👍@meridianbettz
Lydia Emmanuel Magoti
Yupo sahii Bale nimemkubali jembe Hilo lakujiamin
Mwanahamisi
Bale Yuko poa
Dorophina
Bale namkubali sana yupo vizuri
Johnmary joel
Huyo mwamba#meridianbett
Rehema
Bale Yuko fresh tu
Khadija
bale yupo vizuli sana#meridianbettz
Antony Luseno
Mwisho wa siku kiendacho mfukoni ndo cha msingi
Povel
Bale natumain msimu huuu unawez hukawah mwisho wake pale santiago bernabue kikubw kinachomwek pale ni pesa tu hakun kngne natumain mkataba ukifikah tamati atatafuta timu ya kucheza leo
Neema
Bale namkubalii
Sauda
Bale hana mpinzani
Samira
Bale ni mchezaji mzuri sana sema madrid hawataki kumpa nafasi ila cha kupoteza hana kabisa
aisha
Nadhani mshahara anaolipwa pale madrid hata asipocheza yeye kwake poa tu.
Gabriel
Bale yuko vzur sana namkubal Ingawa zipo klabu zinazomhemea, sioni kikosi chochote kati ya hivyo vinavyowania maarifa yake kinachoweza kumudu bei yake. Ni pigo kubwa sana kwamba kwa sasa hajakuwa akiunga kikosi cha kwanza cha Real. Licha ya kuhangaishwa huko, hatahiari kuondoka akasema Barnett.
Kufikia sasa, Bale anajivunia kufungia Real zaidi ya mabao 100 na kushindia miamba hao wa soka ya Uhispania mataji manne ya La Liga nkubal sana huyu jamaa
Theonestina
Namkubar Sana Bale
Venerose
Bale yuko pouwa
Shafii
Licha ya kuambiwa kwamba hayupo kwenye mipango ya zidane ila bale anaangalia pesa clubuni hapo anazolipwa.
Omary lukumbi
Duu pesa si mchezo ata akae benchi kwa kiasi gan pesa tuu ndio ilitawala kichwan kwake
Agness
Bale Yuko vizuri
Amiri Kayera
Bale nais amelizk maish ya pale
Janeflora malisa
Bale yupo vzr
Furahav
Daah wameshamchoka sasa.
Hope mwaikuka
Bale nmekukubali mwanang umetishaa n hyo ndo akili sasa
Shan
Mwache ale pesa zake bale
JULIANA
Asante kwataharifa
Sadick
Sio yeye tu hata Wayne Bridge alifanya hivyo akiwa Man City na Chelsea na hakujali#meridianbettz
Saupha mohamed
Bale yupo vizuri sana
jullie
bale yuko vizuri
lombo
Asante meridianbet kwa makala bomba
Genia Sikaluzwe
Jamaa mzuri sana
Issa
Piga pesa bale
Rose kapinga
Bale Kama bale wakuachee!!
Ester jackson
Bale nahisi yeye nikama mwanafuzi ambae hataki shule lakini ameingia kwenye mtihani wewe unafikiri atajaza nini ndiyo bale hapendi kwenda klabu nyingine kwa sababu anataka kupata hela hiyo mana ni nyingi sana ila kama real Madrid wasipo muongezea mkataba basis mkataba wake ukiisha atakuwa mchezaji huru ila itakuwa amewanyoosha real
felister
Mimi nadhani kikubwa mkono umeenda kinywani
Devotha
Bale yupo vizuri
Sabrina
Asante kwa taarifa
Zeiyana
Kwa maelezo hayo bale yupo sahihi sana ni kweli pesa ndio kila kitu katika maisha haya ya sasa na ukiangalia bale yupo vizuri sana na kama akimua kwenda clabu yoyote hanakubaliwa
warda
Bora abaki bwana
David Pere
Safari ya bale inafurahisha sana real madrid kwa mimi naona kama atamaliza na nao real madrid arudi nyumbani ili kuongeza chachu ya ushindani so naona arudi tottenham