Nottingham Forest inayotumia pesa nyingi iko tayari kuongeza kikosi chao cha wachezaji mwezi huu huku Steve Cooper akifichua kuwa Jesse Lingard atakuwa nje ya uwanja kwa mwezi mmoja.

Cooper anaamini klabu hiyo itafanya kila juhudi kuimarisha kikosi chake kabla ya harakati za kuhakikisha usalama wa Ligi Kuu ya Uingereza wa kushuka daraja.
Nottingham ilisajili wachezaji 21 katika dirisha lililopita la uhamisho, wakati wa majira ya kiangazi ya Uingereza, huku mchezaji huru Serge Aurier baadaye akijiunga na wingi wa waliowasili baada ya muda wa mwisho wa mikataba kupitishwa kati ya vilabu.
Ilikuwa ni shughuli isiyo ya kawaida kutoka kwa timu iliyopandishwa daraja, kurejea ligi kuu ya Uingereza kwa mara ya kwanza tangu 1999, na wamedhamiria kuhakikisha kwamba hawashuki daraja.

Baada ya sare ya 1-1 hapo jana dhidi ya Chelsea, ambapo Aurier alifunga, Cooper aliulizwa kuhusu uwezekano wa kusajili wachezaji wapya, na akasema: “Nadhani hivyo, natumai hivyo.
“Nina imani na klabu kufanya kazi, na ikiwa kuna mambo ambayo yanaweza kusaidia kikosi na timu na kile tunachohitaji, basi tutafanya hivyo. Na kuna hisia ya timu yetu kusajili wachezaji tena, lakini majira ya joto yalikuwa majira ya joto, lazima uangalie tulipo sasa.”
Nottingham inashika nafasi ya 18 kwenye Ligi Kuu yenye timu 20, huku timu tatu zikiwa zinashuka daraja mwishoni mwa msimu. Cooper alithibitisha kiungo wa kati wa zamani wa Manchester United na Uingereza Lingard hatapatikana kwa mechi kadhaa kutokana na tatizo la misuli ya paja.

Kocha huyo aliiambia Sky Sports kuwa; “Tumepokea majeraha ya muda mrefu tangu majira ya kiangazi kwa wachezaji muhimu. Jesse yuko nje kwa mwezi mmoja sasa na ikiwa tunaweza kuongeza wachezaji wanaofaa katika nafasi zinazofaa, basi tutahitaji kufanya hivyo, na tutataka kufanya hivyo pia.”


