Novatus Kaka! Shika simu yangu, ingia kwenye Notebook yangu kuna majina nimeandika hapo, hayo yote ni kwa ajili yako maana tunaishi kwa mifano, hilo jina la kwanza ni Renato Sanchez wa Ureno
Huyo Mtoto alikuwa Golden boy 2016, dunia yote ilikuwa miguuni mwake bahati mbaya sana presha ikambeba, uzito wa jina ukamuhukumu mwisho ukubwa wa Bayern Munich ukapigilia msumari wa mwisho, najua unakumbuka kilichotokea
Nenda na jina la pili hapo, umesema ni Bojan Kirkic Perez! Naam pale Joan Gamper Barcelona alikuwa anafanya mazoezi pembeni ya Lionel Messi, alifanya maajabu makubwa na dunia ikamsubiri
Alifunga kila weekend pale Camp Nou, alicheza atakavyo na tukaamini La Masia imeleta kitu, ila ujana maji ya moto bwana Novatus, mtoto huyu ukubwa wa jina lake ukamchukua, akili ikajifumba maisha yaliisha alivyotoka tu Camp Nou
Umesema umeliona jina lingine hapo la Kylian Mbappe! Naam huyu dunia ilianza kuwa chini ya miguu yake tangu Monaco akaitwa The Second Prince, licha ya ukubwa wake alikuwa analala hostel na kudamka mazoezini
Leo hii Mbappe kashinda vingi lakini bado anahitaji vingi, ukubwa wa jina lake kauficha nyuma, bado anajiona Mbappe mtoto mdogo asie na kitu kwenye dunia, Bwana Novatus kuna somo hapa
Nisiwe muongeaji sana, kwa Renato nakupa somo utaanguka ila futa vumbi simama tena, kwa Bojan ni majuto ni mjukuu na kwa Mbappe ni endelea kupambana kuwa jua ili ukidondoka uwe nyota tu.
Hii ni halisi kwa ajili ya mashujaa wote! Ukiwa jasiri unavuna mkwanja kibao hapa na sloti hii ya Huangdi Casino. Waka nusu tukupe maradufu!
Povel
The meridian bet kwa makala nzuri ya kispoti ya wasihiii wachezaj wetu kuwa na nidhamu katika maisha ya soka kwani muda haumsubir mtu na majuto baadaye sana
Hopemwaikuka
Kabsaa yaan
Sabrina
Ni kweli kabisa yani
Issa
Mpira ni kujituma sana ili ufike unapotaka
Dorophina
Mwandishi ameongea uharisia kabisa Sanchez ni kiboko mwaka huo
warda
Ndo mana kwenye suala la mpira unatakiwa kujituma sana ukiwa bado unanguvu
Shani
Soka c kitu cha masihara ni kujitoa mazima
Sauda
Sahihi kabisa
Adelta
Mashabiki tumeielewa makala
Khadija
Mpira ni kujituma sana ukiwa uwanjani hili kureta hamsha hamsha kwa mashabiki
Mwajumah
Alichosema Novatus ni sahihi kabisa
Tatu
Nikweli mpira ni kujituma na nidhamu ni ndio kila kitu
Fatina mfigi
Mpira Ni kujituma na kuweka nidhamu ya kutosh nje ya uwanj na ndan pia
Caroline
Asante sana kwa uchambuzi yakinifu
aisha
Mchezaj anatakiw ajitume zaid
Ester jackson
Good