Siku ya jana Rais mstaafu wa Marekani, Barack Obama alikuwa kwenye mazungumzo ya mtandaoni mshambuliaji kinda wa Manchester United, Marcus Rashford na Obama ameoneshwa kufurahishwa na jitihada za Rashford na kumpa hongera.
Mazungumzo hayo yalilenga vitu vingi huku kila mmoja akieleza uzoefu wake kutoka kwenye shughuli za kila siku na jitihada za kupambana na umaskini. Obama alieleza wazi kuvutia na jitihada anazotenda Rashford za kujaribu kusaidia maskini.
Licha ya hilo, Obama ameleza kuwa Rashford ameonesha ukakamavu sana kwani katika umri wa miaka 23 aliyokuwa nayo kinda huyo.
Hivi karibuni mchezaji huyo alipewa heshima rasmi na kujumuishwa miongoni mwa wanachama wa ufalme wa Uingereza kutokana na mradi wake wa kusaidia watoto kupata chakula mashuleni kufanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Rashford alipewa cheo cha MBE yaani MEMBER OF BRITISH EMPIRE, cheo alichopata kutokana na namna amepambana kuhakikisha serikali inabadili sera zake kwa Wanafunzi kupata chakula bure Mashuleni, cheo hicho hutolewa kwenye siku ya kuzaliwa ya Malkia Elizabeth.
BONASI YA 50% KILA SIKU KATIKA KASINO ZA EVOPLAY HAPA MERIDIANBET.
Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.
Rashford yupo vizuri Sana Kila mtu lazima amkubali
Rashford yuko vizuri
Rashford jembe