Ole Gunnar au Klopp: Nani Alidunda Vibaya Wikiendi?

Ligi ya Kuu Uingereza imeendelea kunoga huku mabingwa wa Ligi msimu uliopita wakilazwa chali kwa mvua ya magoli dhidi ya Aston Villa wikiendi. Manchester United naye alikalia kuti kavu kwa kuruhusu kichapo cha Spurs.

Wikiendi hii ulikuwa ni wakati wa Mourinho kulipa kisasi kwa klabu yake iliyomtimua kazi akiwatandika bao 2-6, kipigo ambacho hakikutarajiwa kabisa kwa Man United kupigwa wakiwa nyumbani.

Mechi iliyoshitua zaidi wapenzi wa soka, na ambayo inaweza kuwa imechana majamvi ya watafutaji makini wa mkwanja kwa kubashiri ni mechi dhidi ya Liverpool. Hakuna aliyetarajia mabingwa kuchapwa 2-7 kama walikuwa wamesimama uwanjani.

Safari ya kipigo ya Man United imeanza dakika ya 4 ya mchezo baada ya Tanguy Ndombele kusawazisha goli la penati lililofungwa na Bruno Fernandes dakika ya pili. Kisha Heung-Min Son akafunga magoli 2,  Harry Kane 2, Serge Aurier 1. Anthony Martial alipata kadi nyekundu dakika ya 28. Kipindi cha kwanza kiliwaacha Man U na deni la magoli matatu zaidi, na wakashindwa kufurukuta kipindi cha pili na kumaliza kwa kichapo cha 2-6.

Kwa upande wa Liverpool, wao walianza kuchezea kichapo dakika ya 4 pia, wakifungwa goli lao la kwanza. Kipindi cha kwanza kimeisha Liverpool wakiwa wamechapwa bao 4-1, kipindi cha pili waliambulia goli 1 jingine na kuruhusu Villa kuwapa burudani ya goli 3 zingine. Wikiendi imeisha vibaya kwa mabingwa hawa.

Matokeo ya Jumla Ligi Kuu Wikiendi

Oktoba 3, 2020

Oktoba 4, 2020


 

Weka  Pesa kwa Airtel Money!

Sasa unaweza kuweka pesa moja kwa moja kwenye akunti yako ya Meridianbet kwa kutumia mtandao wa Airtel. Usipate wasi wasi, tunaifanya kazi kuwa rahisi zaidi!

Soma Zaidi

31 Komentara

    Asanteni kwa taarifaa meridianbet.

    Jibu

    Asnt kwa taarif

    Jibu

    Liverpool walijiamini sana wakaona wanacheza na timu ambayo ilikuwa hatarini kushuka daraja na kusahau kuwa mchezo unaweza kubadilika mda wowote ule dimbani poleni sana man u na Liverpool mana wote mko sawa

    Jibu

    🤣🤣🤣 lakini naogopa

    Jibu

    Hakuna wa afadhari wote wamepata kichapo cha mbwa koko

    Jibu

    Hamna kitu hapo

    Jibu

    hakuna ata mwenye nafuu maana wote walichezea kichapo cha aibu sana

    Jibu

    Mourihno kaokota dodo kwenye muarobaini kwanza man u haina kikosi kizuri alafu mourihno kashaitumikia sana ile clabu so haikua kazi ngumu sana kwake..!kwa upanda wa Liverpool naona hunafika mwisho wa klopp kusepa siku zote kutesa kwa zamu zamu yao hishakwisha Liverpool

    Jibu

    Hamna jambo hapo

    Jibu

    Wapo hoi hawana jipya wajipange tuu!!!

    Jibu

    Pole yao

    Jibu

    Ilikuwa weekend ya matokeo ya kushangaza kweli kweli#meridianbettz

    Jibu

    Hamna kitu apo

    Jibu

    Kloop alidunda vibaya

    Jibu

    Klopp kalala doloooo

    Jibu

    Walijisahau sana

    Jibu

    Dah villa on fire pengo la mane linaonekana waz liverpool

    Jibu

    Vipgo vya fedhea sana

    Jibu

    Kloop mtu mbaya sijui ka kwama wapi

    Jibu

    Aibu babu 😂

    Jibu

    Weekend ya kibabe sana hiii

    Jibu

    Ilikuwa no kuchekana na vibes kama lote

    Jibu

    Ilikua ya motooo

    Jibu

    Wote wameambulia kichapo

    Jibu

    Liverpool walijiamini sana wakaona wanacheza na timu ambayo ilikuwa hatarini kushuka daraja na kusahau kuwa mchezo unaweza kubadilika mda wowote ule dimbani poleni sana man u na Liverpool mana wote mko sawa

    Jibu

    Kichapo cha klopp kilikuwa cha mbwa koko

    Jibu

    Duuh

    Jibu

    Du nouma Sana

    Jibu

    Watoto wadogowamewatoa jasho

    Jibu

    Awachekan wote

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.