Imekuwa ni jambo la kawaida kwa wamiliki wa timu kufanya maamuzi magumu pale ambapo wanaona mwenendo wa vikosi vyao hauendi sawa na kile ambacho wao wanakitarajia baada ya kuweka fungu fulani kwa ajili ya kusaidia vikosi vyao kusonga mbele na kunyanyua mataji mbalimbali.
Pale inapokuwa tofauti na matarajio yao basi uongozi huchukua maamuzi magumu kuwaondoa wakufunzi ambao ndiyo chachu ya upatikanaji wa matokeo mazuri mara baada ya kuwaamini na kuwapa mahitaji ya wachezaji ambao hutokea kuwahitaji katika kujenga na kuimarisha vikosi vyao.
Sylvinho ni miongoni mwa makocha wenye historia ya pekee ndani ya soka lakini ameshindwa kupata matokeo mazuri katika ligi mara baada ya kuondoshwa katika klabu ya Lyon. Ni mapema sana kuondoshwa klabuni hapo ikilinganishwa na muda ambao alijiunga kukinoa kikosi hicho.
Mapema Mei, alianza safari yake ya kunoa kikosi cha Lyon lakini hajafaidi lolote ndani ya maisha hayo katika jiji la Ufaransa mara baada ya kushindwa kufikia lengo ambalo kikosi hicho kimejiwekea na pia kuweza kuhakikisha anaifikisha klabu hiyo katika hatua ya juu kabisa kwenye kinyang’anyiro cha mataji.
Amekuwa na mlolongo mbovu wa matokeo katika ligi mara baada ya kuondoka na ushindi katika mechi moja pekee ndani ya mechi tisa ambazo aliingia uwanjani na kikosi chake. Hatua hiyo ilikuwa ngumu kuvumilika kwa kikosi ambacho kimejenga jina na heshima yake kwa miaka mingi kuendelea kupokea kipigo cha aina hiyo.
Wengi walihisi Mbrazil huyo angekuwa na mafanikio makubwa baada ya kuanza kampeni yake ya ligi kwa kuwa na ushindi mkubwa mbele ya Angers na Monaco ila mambo yakawa tofauti kabisa na vile ambavyo walitarajia. Kutokana na hilo imelazimu waweze kumuacha apishe nafasi kwa ajili ya wengine kunusuru safari ya kikosi hicho.
Majukumu hayo mazito kwa sasa anakabidhiwa kocha msaidizi wa kikosi hicho mara baada ya kuona kwamba ni mtu pekee ambaye anaweza kuendesha gurudumu hilo huku klabu ikijipanga kupata mtu atakayeshika kikosi hicho kwa muda mrefu zaidi na siku za mbeleni.
Furahav
Habari nzuri