Kiungo wa Senegal, Pape Gueye, ametangaza kuwa atachukua mapumziko ya kuichezea timu ya taifa kufuatia kuondolewa kwa Senegal kwenye Taji la Dunia 2026.
Gueye amesema atazungumza kwa kina kuhusu kilichosababisha kuondolewa kwa timu hiyo siku zijazo, lakini kwa sasa amesisitiza kuwa hatarudi kuichezea Senegal kwa muda wote ambao benchi la sasa la ufundi litaendelea kuiongoza timu.Kauli hiyo imezua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki wa Senegal, huku wengi wakisubiri kuona kama kutakuwa na mabadiliko ndani ya benchi la ufundi au kama kiungo huyo atabadilisha msimamo wake siku zijazo.
Jana hakufurahishwa kutolewa na nafasi yake ilichukuliwa na Lamine Camara. Mchezo ulimalizika kwa wao kupoteza kwa mabao 3-2 licha ya kuongoza 2 bila mpaka dakika ya 84.




